SERIKALI
 inatekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano 
(2016/17- 2020/21) unaolenga katika kuimarisha ustawi na maendeleo ya 
jamii kwa kuongeza upatikanaji wa huduma bora za jamii ikiwemo elimu, 
afya na maji.
Ili
 kufanikisha malengo hayo, Serikali imeweka utaratibu wa kukusanya 
taarifa muhimu za wananchi wake kupitia takwimu mbalimbali ili kuweza 
kupanga mipango ya maendeleo.
Taarifa
 hizo zinazotolewa katika mfumo wa takwimu ikiwemo hali ya vizazi na 
vifo nchini zinalenga katika kuanisha mahitaji halisi ya wananchi ili 
kurahisisha uandaaji wa sera na mipango ya maendeleo kulingana na 
mahitaji na mazingira yaliyopo
Pamoja
 na jitihada hizo inaelezwa kuwa mfumo  wa usajili, utambuzi na uwekaji 
wa kumbukumbu wa matukio muhimu ya binadamu  ikiwemo vizazi, vifo, ndoa,
 talaka na hati za uasili wa watoto umekabiliwa na changamoto mbalimbali
 kutokana na mifumo ya sheria zilizopo.
Inaelezwa
 kuwa matukio mengi yanatokea katika ngazi za vjiji, vitongoji, mitaa na
 kata ambapo watendaji na viongozi wa mamlaka husika wanatambua uwepo 
wake yameshindwa kuingizwa katika taarifa rasmi kutokana na  Sheria za 
Serikali za Mitaa kutowapa jukumu la kusajili na kutunza takwimu za 
matukio hayo.
Wizara
 ya Katiba na Sheria kupitia Wakala wa Usajili, Ufulisi na Udhamini 
(RITA) inatekeleza Mkakati wa Taifa wa Usajili wa Matukio Muhimu ya 
Binadamu na Takwimu (CRVS) ambao unalenga kuimarisha shughuli za usajili
 wa matukio muhimu na upatikanaji wa takwimu muhimu kwa maendeleo ya 
nchi.
Kupitia
 Mkakati wa CRVS Wizara imedhamiria kukuza na kuendeleza matumizi ya 
TEHAMA katika usajili wa vizazi na vifo ambapo tayari imezindua mfumo wa
 kielektroniki wa usajili wa vizazi na vifo kwa kuzingatia mahitaji 
ambao ulianza kufanya kazi rasmi mwezi Novemba, 2017.
Akiwasilisha
 Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19, 
Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi anasema katika 
kipindi cha mwaka 2017/18, jumla ya vizazi 1,593,313, vifo 46,914, ndoa 
15,866, talaka 91 na hati 44 za watoto wa kuasili zilisajiliwa nchini.
Anaongeza
 kuwa Kupitia mradi huo wananchi wanapata huduma za usajili wa vizazi na
 vifo kupitia ofisi za kata, vituo vya afya na hospitali, ambazo kwa 
kawaida zipo karibu na wananchi walio wengi, na vyeti vya kuzaliwa na 
kifo vinatolewa papo hapo.
“Hii
 ni ongezeko la usajili wa vizazi 201,110, vifo 9,038, hati za watoto wa
 kuasili 10 na talaka 69 ikilinganishwa na matukio yaliyosajiliwa katika
 kipindi kama hicho kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 isipokuwa ndoa ambayo 
ni pungufu ya ndoa 1,907” anasema Prof. Kabudi.
Kwa
 mujibu wa Prof. Kabudi anasema jumla ya vizazi 929,938 vilisajiliwa na 
kupatiwa vyeti vya kuzaliwa kupitia Mpango wa Usajili wa Watoto walio 
Chini ya Miaka Mitano na kufanya kiwango hicho kwa Tanzania Bara 
kuongezeka kutoka asilimia 13 mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 28 mwaka 
2017 sawa na ongezeko la vizazi 2,673,806.
Prof.
 Kabudi anasema Ongezeko la usajili wa matukio ya vizazi na vifo ni 
kielelezo kuwa RITA imejiimarisha katika kusajili matukio muhimu ya 
binadamu na kuwataka wananchi kutoa taarifa za matukio hayo katika 
mamlaka mbalimbali.
Akifafanua
 zaidi Prof. Kabu vizazi 63,550 vimesajiliwa na kupatiwa vyeti vya 
kuzaliwa kupitia Mpango wa usajili wa watoto walio shuleni katika Mkoa 
wa Njombe.
Prof.
 Kabudi anasema kupitia mfumo huo RITA itaweza kubadilishana taarifa na 
mifumo mingine ya usajili kama Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Mamlaka ya 
Vitambulisho vya Taifa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Idara ya Uhamiaji 
kwa ajili ya kuziwezesha taasisi hizo kufanya maamuzi sahihi, kwa wakati
 na kwa gharama nafuu.
Anasema
 kuwa kufuatia taarifa ya utafiti ya mfumo wa Sheria ya Usajili wa 
Matukio Muhimu ya Binadamu iliyoandaliwa na Tume ya Kurekebisha Sheria 
Tanzania kwa kushirikiana na RITA, Wizara yake inatarajia kuwasilisha 
Bungeni Muswada wa Sheria ya Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu ili 
kuwezesha matukio mengi zaidi kusajiliwa.
“Wizara,
 kupitia Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) pamoja na Tume ya
 Kurekebisha Sheria Tanzania, imefanya maandalizi ya awali ya kufanyia 
utafiti mfumo wa kisheria wa ufilisi nchini ili kuweka msingi wa 
kutungwa upya kwa mfumo wa kisheria wa kuweka mazingira wezeshi ya 
kufanya biashara na uwekezaji nchini” anasema Prof Kabudi.
Ili
 mfumo wa CRVS uweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa, ni wajibu wa taasisi
 za umma kuimarisha na kuwa mfumo mmoja wa wa taarifa na mawasiliano 
katika utambuzi wa matukio mbalimbali ili kuhakikisha kuwa  matukio 
yanaleta manufaa kwa wananchi na Taifa katika kupanga na kutekeleza 
mipango mbalimbali ya maendeleo.






No comments:
Post a Comment