Profesa
 Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili 
wa Vyama vya siasa amesema kuna njama za kukinyima ushindi chama hicho 
katika uchaguzi wa ubunge wa Liwale utakaofanyika Jumapili Oktoba 13, 
2018.
Akizungumza
 na waandishi wa habari leo Jumanne Oktoba 9, 2018, Lipumba amesema 
Liwale ni ngome ya CUF lakini wameanza kunusa harufu ya kupokwa ushindi.
“Mgombea
 wetu Mohamed Rashidi Mtesa anakubalika na tangu achaguliwe kuwa diwani 
kata ya Liwale amefanya mengi na hata kushirikiana na watendaji wa 
Serikali ila kwa sasa  tumeanza kuhisi kufanyiwa rafu, tunaiomba tume 
(Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC)  itende haki," amesema Lipumba.
Amesema
 katika kudhihirisha kuwa Liwale ni ngome ya chama hicho, katika 
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, CUF ilishinda kata 17 na CCM kata saba.
Amedai kuwa CCM inataka kulichukua jimbo hilo kwa nguvu kwa kuwatumia baadhi ya watumishi wa umma.
Amesema
 si vyema Taifa wakati likiadhimisha kumbukumbu ya miaka 19  ya kifo cha
 Mwalimu Julius Nyerere, likaingia kwenye vurugu za uchaguzi Liwale.
“Tufanye
 uchaguzi wa haki ili mshindi apatikane kwa haki. Liwale ni ngome yetu 
na hiyo inatokana na mizizi iliyowekwa na muasisi  wa chama chetu Mzee 
Shaban Mloo.
"Mawakala
 wetu wamekula viapo lakini mpaka sasa hakuna hata mmoja aliyepewa 
nakala za viapo hii ni dhahiri kwamba kuna njama ambazo zinafanyika 
kutowapitisha ili wajitangazie ushindi kwa kuiba kura" 
"Tunamtaka
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi aache mara moja tabia ya kufanya mikutano ya 
hadhara kwa madai anahamasisha maendeleo na kuwataja wanachama wa CUF 
kuwa atawakamata kwa sababu yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na 
Usalama " Amesema Prof Ibrahim Lipumba 
Uchaguzi
 Liwale unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya
 CUF, Zuberi Kuchauka kujiuzulu na kujiunga na CCM. Kuchakua ni mgombea 
wa CCM katika uchaguzi huo.






No comments:
Post a Comment