Serikali
 imeipa changamoto Bodi ya sukari nchini kutekeleza majukumu yake kwa 
weledi ikiwa ni pamoja na kusisitiza kuhuisha uzalishaji wa sukari kwa 
wingi ili kuondokana na uagizaji wa sukari kutoka nje ya nchi.
Kampuni
 mbalimbali za uzalishaji wa sukari nchini zimeitikia wito wa Serikali 
wa kuongeza uzalishaji wa sukari ili nchi iweze kujitegemea kwa bidhaa 
hiyo pendwa kwa matumizi ya nyumbani na viwandani na ziada jambo 
litalopelekea Bodi ya sukari kusimamia majukumu yake ipasavyo ili 
kuondokana na uagizaji wa sukari nje ya nchi.
Kauli
 hiyo imetolewa leo jumatatu tarehe 29 Octoba 2018 na Waziri wa kilimo 
Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb)  wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa 
Bodi ya Sukari Tanzania (SBT) hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Wakala
 wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Mjini Dodoma.
Waziri
 Tizeba amemtaka Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari nchini Bi Mwamini Juma 
Malemi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Prof Kenneth 
Michael Kitundu Bengesi Kudhibiti sukari inayoingia nchini pasina 
utaratibu huku akiwataka kusimamia kwa weledi ufanisi katika uongezaji 
wa uzalishaji wa sukari nchini.
Aidha,
 Dkt Tizeba alisema kuwa ufungashaji wa sukari kwenye ujazo wowote ule 
kwa kutumia vifungashio vya aina yoyote kama vile mifuko yenye nembo ya 
SUPER FINE lazima uzingatie Sheria ya Sukari Namba 26 ya Mwaka 2001 
ambayo inazuia ufungashaji wa sukari bila kupata idhini ya Bodi ya 
Sukari Tanzania.
Alisema
 kuwa kwa mujibu wa Sheria hiyo ni marufuku kufungasha au kuuza sukari 
nyeupe kwa kuwa sukari hiyo ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani kama 
malighafi na sio kwa ajili ya matumizi ya kawaida majumbani.
Alisisitiza
 kuwa Mtu yeyote atakayebainika kuvunja Sheria hiyo ya Sukari, 
atawajibika kulipa faini ya kiasi cha fedha kisichopungua Shilingi 
Milioni Kumi (10,000,000) au kifungo cha miaka mitatu (3) jela au vyote 
kwa pamoja.
“Kuna
 watu wanaolipa kodi ili wazalishe sukari lakini inapoingia sukari 
ambayo imepenya kinyemela hata ulinganifu wa soko madukani unakuwa mdogo
 kwa kuwa wanaoingiza bila utaratibu wanauza kwa kiasi cha chini kwa 
kuwa hawana uchungu wa kulipa kodi”
“Na
 hili sio jambo la hiara Bodi ni lazima isimame kidete kubaini mianya 
yote ya wafanyabiashara wanaoingiza sukari bila utaratibu” Alikaririwa 
Dkt Tizeba
Kuhusu
 sukari ya viwandani (Industial Sugar) Dkt Tizeba alisema kuwa, 
wafanyabiashara wamekuwa wakiomba kiwango kikubwa cha kibali cha 
uagizaji wa sukari lakini serikali ikihakiki kupitia kodi waliyolipa 
inakuwa haifanani na kiasi kilichoagizwa.






No comments:
Post a Comment