Mfanyabiashara Hafidhi Jonggradgorn ametiwa hatiani na madini yake yenye thamani ya Dola za Marekani 105,757.38 kutaifishwa na Serikali baada ya kukiri kosa la kukutwa na madini hayo bila leseni.
Mshtakiwa huyo alihukumiwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.
Mahakama
 hiyo ilimtia hatiani na kumhukumu kwenda jela miaka miwili au kulipa 
faini Sh milioni mbili kwa kosa la kwanza na kosa la pili jela miaka 
mitatu au faini Sh milioni tatu.
Kabla
 ya hukumu hiyo, Wakili wa Serikali, Jackline Nyantori alimkumbusha 
mshtakiwa mashtaka yanayomkabili ambapo alidai anadaiwa kutenda kosa 
kati ya Januari 2017 na Juni 3, 2018.
Nyantori
 alidai shtaka la kwanza mshtakiwa anadaiwa katika maeneo tofauti 
Tanzania na Falme za Kiarabu na India, akiwa si mtumishi wa umma kwa 
makusudi alifadhili biashara ya madini kwa lengo la kupata faida.
Nyantori
 alidai katika shtaka la pili, mshtakiwa katika tarehe hizo maeneo ya 
Mikocheni A, Mtaa wa Chwaku alikutwa na vito vya thamani aina ya 
gamestones kilo 62.76 vyenye thamani ya Dola za Marekani 105,757.38.
Mshtakiwa
 alikiri makosa hayo na kutiwa hatiani na upande wa mashtaka ulitaka 
apewe adhabu kwa mujibu wa sheria kwa sababu mshtakiwa ameingilia 
maliasili za taifa.
“Mheshimiwa
 Hakimu tunaomba madini yataifishwe yakabidhiwe serikalini chini ya Tume
 ya Madini, bastola arejeshewe mshtakiwa,” alisema Nyantori.
Akijitetea
 mbele ya hakimu, mshtakiwa huyo aliomba apunguziwe adhabu kwani ana 
familia na watoto wameshindwa kwenda shule kwa sababu ya kukosa ada, ni 
mfanyabiashara anayeipa Serikali kipato.
Hakimu
 Mashauri alisema mshtakiwa mbinu anayotumia inaikosesha Serikali 
mapato, hivyo alimuhukumu kwa kosa la kwanza faini Sh milioni mbili au 
kwenda jela miaka miwili.
Alisema kosa la pili faini Sh milioni tatu au jela miaka mitatu.
Hata hivyo mshtakiwa hajalipa faini hivyo amekwenda jela.






No comments:
Post a Comment