Zoezi
 la kununua nafaka ya mahindi kwa ajili ya akiba ya Taifa ya Chakula 
unaendelea katika maeneo mbalimbali kote nchini ambapo wakulima kwa 
kiasi kikubwa wameitikia wito uliotolewa na Wakala wa Taifa wa hifadhi 
ya chakula (NFRA) wa kutonunua mahindi yasiyokuwa na ubora.
Pamoja
 na Ubora wa mahindi kuwa changamoto katika maeneo mengi nchini kutokana
 na hali ya msimu wa mwaka Jana kuwa na jua Kali na mvua za msimu jambo 
lilolopelekea Mazao kuharibika yakiwa shambani.
Katika
 hatua nyingine Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi 
ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia L. zikankuba ameendelea na ziara ya kikazi 
ya kutembelea vituo mbalimbali vya ununuzi ambapo hivi tarehe 1 Octoba 
2018 alitembelea kituo cha ununuzi cha Kigonsela kilichopo Mkoani Ruvuma
 kukagua mwenendo wa zoezi la ununuzi katika kituo hicho.
Katika
 ziara hiyo ya Mtendaji Mkuu wa NFRA mkoani Ruvuma, Meneja wa Kanda ya 
Songea Ndg Amos Mtafya alieleza kuwa Kanda ya Songea pekee imepangiwa 
kununua jumla ya tani 7, 000 kwa awamu ya kwanza ya ununuzi na hadi 
kufikia leo tarehe 1 Oktoba 2018 Kanda hiyo imeshanunua zaidi ya tani 
6000. 
Ili
 kuimarisha dhana ya Ushirika, Wakala umenunua kwa kiasi kikubwa mahindi
 kupitia vyama ya Ushirika na vikundi vya wakulima yaani SACCOS na AMCOS
 ambazo jumla yake zinakuwa 23 ambazo ndizo zilizobainishwa na uongozi 
wa Mkoa wa Ruvuma. 
Vikundi
 hivyo vya wakulima ni kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, 
Songea vijijini, Mbinga mji, Mbinga vijijini,  Namtumbo na Wilaya ya 
Nyasa.
Vumilia
 alionyesha kuridhishwa na hali ya ubora wa nafaka iliyonunuliwa na 
kuwahimiza watumishi wa NFRA kuendekea kusisitiza na kununua mahindi 
yenye vigezo vya ubora unaokubalika kwa ajili ya Hifadhi ya Taifa ya 
Chakula.
Katika
 hatua nyingine Bi Vumilia amewapongeza watumishi wa NFRA kwa kazi nzuri
 ya kiuweledi wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao na wakala kwa 
ujumla.






No comments:
Post a Comment