Mkazi 
 wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, Msema Msafiri maarufu kwa jina la 
Giriki (35), ameliwa na mamba, alipokwenda katika mwambao wa Ziwa 
Tanganyika kuogelea.
Imeelezwa
 kuwa Msafiri, mkazi wa Kitongoji cha Lyela kilichopo mwambao wa Ziwa 
Tanganyika katika Kijiji cha Izinga Kata ya Wampembe, alikwenda kuogelea
 kutokana na joto kali alilokuwa akilihisi.
Alikumbwa na mkasa huo Ijumaa majira ya mchana, baada ya kuingia ziwani na kuanza kuogelea.
Akizungumzia
 tukio hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Izinga, George Fataki, alisema 
kuwa kijana huyo alikuwa ni mgeni katika kitongoji hicho na alikuwa 
ametokea mkoani Kigoma katika Kijiji cha Kalago na kwenda katika katika 
kitongoji hicho ambacho ni makazi ya wavuvi mwezi mmoja uliopita, kwa 
lengo la kufanya shughuli hizo.
Alisema
 kwa kuwa mazingira aliyotoka yalikuwa na baridi, hivyo mazingira ya 
ziwani yalikuwa yakimsumbua kutokana na joto kali, kitendo 
kilichosababisha ajenge mazoea ya kwenda kuogelea ziwani.
Kwa
 mujibu wa Fataki, siku ya tukio hilo majira ya saa 8 mchana aliwaaga 
wavuvi wenzake kuwa anakwenda kuupoza mwili kwa kuogelea ziwani na 
alipofika aliingia ndani ya maji na kuanza kuogelea, ghafla aliibuka 
mamba na kumvutia katika kina kirefu cha maji na kuanza kumla kisha 
kuondoka naye.
Mwenyekiti
 wa kijiji hicho alisema kuwa baadhi ya wavuvi walikuwa wanashuhudia 
tukio hilo kwa mbali, lakini walishindwa kutoa msaada, hivyo mamba huyo 
kuondoka na Msafiri na mpaka sasa jitihada za kuutafuta mwili wake 
zinaendelea.
Kamanda
 wa Polisi mkoani Rukwa, George Kyando, alithibitisha kutokea kwa tukio 
hilo na kuwatahadharisha wananchi wanaoishi maeneo ya mwambao mwa ziwa 
na mito kuacha tabia ya kwenda kuogelea, kwa kuwa ni hatari kwa usalama 
wao.






No comments:
Post a Comment