Naibu
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amewataka 
viongozi kuanzia ngazi ya mkoa hadi vijiji nchini kuhakikisha wanafunzi 
wanaomaliza darasa la saba hawaondoki katika maeneo yao kwenda kufanya 
kazi za ndani wakati wakisubiri matokeo ya kuhitimu darasa la saba.
Ole
 Nasha ametoa agizo hilo mkoani Manyara wakati akizungumza na viongozi 
hao kuhusu hali ya Elimu mkoani humo ambapo amewataka kusimamia kwa 
ukaribu suala hilo ili kutokatisha ndoto za watoto hao na kwamba wale 
wanaofanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
“Hakikisheni
 watoto wanaposubiri matokeo hawasafirishwi kwani wanapofika huko 
wanarubuniwa na waajiri hivyo hata matokeo yakitoka na kuonesha kuwa 
wamefaulu hawarejei kuendelea na masomo “ alisisitiza Naibu waziri Ole 
Nasha.
Kiongozi
 huyo ameendelea kuwasisitiza wazazi kuwa fursa za Elimu katika nchi 
yetu ni kubwa, ikizingatiwa kuwa Elimu msingi ni bure hivyo hakuna 
kisingizio tena kuwa mtoto hawezi kusoma.
“Wazazi
 msiwe sehemu ya kuchangia watoto wenu kwenda mjini kwa kuwa tu 
wanawatumia fedha kwa ajili ya matumizi bali hakikisheni mnawasimamia 
vyema watoto hao katika kipindi chote cha kusubiri matokeo na kuwapeleka
 shule pindi matokeo yanapotoka na kuonekana wamefaulu,” alisisitiza 
Naibu waziri Ole Nasha.






No comments:
Post a Comment