MAHAKAMA
 ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema haiwezi kifuta kesi ya utakatishaji wa 
fedha inayomkabili Rais wa Klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wake 
Godfrey Nyange maarufu Kaburu sababu kesi hiyo imeishafikia hatua ya 
usikilizwaji wa awali.
Badala
 yake Mahakama kwa mara nyingine, imetoa amri na kuwapa siku 14 upande 
wa mashtaka kutekeleza amri iliyoitoa ya kuwataka aidha wafute mashtaka 
dhidi ya Zacharia Hanspoppe na mfanyabiashara, Franklin Lauwo au 
wabadilishe hati ya mashtaka kwa kuwaondoa washtakiwa hao ili kesi 
isikilizwe.
Uamuzi
 huo umetolewa leo mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, 
kutokana na ombi la mawakili wa washtakiwa hao wakiongozwa na Nehemia 
Nkoko kuiomba mahakama ifute kesi hiyo kwa sababu upande wa mashtaka 
wameshindwa kuiendesha.
Akisoma
 uamuzi huo hakimu Simba amesema amepitia hoja za pande zote mbili na 
ameona kuwa, huu si muda muafaka wa kufuta kesi hiyo kwa sababu tayari 
ilikuwa katika hatua ya (PH) na pia ilishatoa amri ambayo bado 
haijatekelezwa.Hakimu Simba amesema upande wa mashtaka wanatakiwa 
watekeleze amri iliyotolewa Mei 12 mwaka ,2018, kwa hiyo haiwezi kufuta 
kesi hiyo, kwa sababu itafuta hadi amri ambayo tayari ilishaitoa na 
haijatekelezeka.
"Si
 muda mwafaka wa kufuta kesi hii, natoa siku 14 kuanzia kesho kwa upande
 wa mashtaka kufanya mabadiliko na kama hawatafanya hivyo, Mahakama 
inaweza kuamua vingine itakavyoona inafaa, " amesema Hakimu Simba.Aidha 
Hakimu Simba ametaka amri hiyo itekelezeke kwa sababu hawajulikani ni 
lini Hansoppe na Lauwo watakamatwa  wakati Aveva na Kaburu wapo 
mahabusu.
Kesi
 hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 16 mwaka 2018 kwa ajili ya washtakiwa 
kusomewa PH.Awali, Wakili wa utetezi, Nkoko aliomba Mahakama hiyo 
iwafutie mashtaka, washtakiwa hao kwa sababu wameshindwa kuiendesha kesi
 hiyo.Akijibu hoja hiyo, wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa 
Kishenyi akisaidia na Wakili kutoka Takukuru, Leonard Swai,  aliiomba 
mahakama kutupilia mbali maombi hayo kwa sababu bado wanaifanyia kazi 
amri waliyopewa na mahakama ya kumtafuta Hanspope na Lauwo.
Amedai
 Septemba 14 mwaka huu, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia 
Jenerali John Mbungo aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza
 kuwa wanawatafuta Hanspope na Lauwo jambo ambalo ni moja ya utekelezaji
 wa amri iliyotolewa na mahakama.
Katika
 kesi hiyo washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 10 likiwemo la kula 
njama, matumizi mabaya na kughushi nyaraka ikionyesha Klabu ya Simba 
inalipa mkopo wa USD 300,000 kwa Aveva kitu ambacho sio kweli.






No comments:
Post a Comment