Marwa Itembe (28), mkazi wa kijiji cha Mbalimbali wilayani Serengeti Mkoa wa Mara amefikishwa mahakamani kwa makosa matatu ya uhujumu uchumi.
Mbele
 ya Hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Serengeti Ismael Ngaile, mwendesha 
mashtaka wa Polisi,  Paskael Nkenyenge jana Jumanne Oktoba 9, 2918 
alisema  mshtakiwa alikamatwa na miguu miwili ya nyumbu yenye thamani ya
 Sh1.4milioni.
Akisoma
 hati ya mashitaka katika kesi ya uhujumu uchumi namba 111/2018 alisema 
kosa la kwanza ni kuingia ndani ya hifadhi ya Taifa, la pili ni  
kupatikana na  silaha za jadi panga na kutega wanyamapori  ndani ya 
hifadhi kinyume cha sheria.
Alisema
 kosa la tatu ni kumiliki nyara za Serikali baada ya kukutwa na  miguu 
miwili ya mnyamapori huyo ikiwa na thamani ya Sh1.4milioni kinyume cha 
sheria.
Ametenda makosa hayo Oktoba 7, 2018 katika eneo la Nyamburi ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mshtakiwa huyo hakutakiwa kujibu chochote na  amerudishwa mahabusu hadi Oktoba 23, 2018 kesi hiyo itakapotajwa tena.






No comments:
Post a Comment