Tanzania
 ni ya pili kwa Urithi wa Maliasili baada ya Taifa la Brazil la Bara la 
Amerika ya Kusini kwa kuwa na vivutio vingi vya Asili.
Hayo
 yameelezwa leo wakati wa ufunguzi rasmi wa Tamasha la Urithi Wetu 
(Urithi Festival)  linalofanyika katika viunga vya Kijiji cha Makumbusho
 Jijini  Dar-es –Salaam na Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama
 vya Wadau wa Utalii Tanzania,  Bwana  Abdukadir Luta Mohamed.
Amesema
 kuna vivutio vingi vya  urithi wa utamaduni, ukiweka pamoja vivutio vya
 utalii wa asili na utamaduni, Tanzania inaweza kuongoza kwa kuwa na 
vivutio vingi vya utalii  duniani.
Bwana Mohamed  amevitaja baadhi ya vivutio hivyo  kuwa pamoja na tamaduni, makabila, mila, desturi, vyakula na Malikale.
Awali
 akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Kamati ya
 Maandalizi ya Tamasha la Urithi Kitaifa, Profesa Audax Mabula ameeleza 
kuwa Tanzania inajivunia kuwa na lugha kuu nne zilizopo Barani Afrika.
Amezitaja
 lugha hizo kuwa ni Wabantu ambao inawajumuisha makabila kama vile 
Wasukuma, Wajita na Wanyamwezi, Wanailotiki inawajumuisha Wamaasai, 
Wakushitiki-inayojumuisha  Wairaq,Wambulu, Wakhoisan –inayowajumuisha 
Wahadzabe na Wasandawe.
Profesa
 Mabula ameeleza kuwa, Kabila la Wasandawe limeanza kupotea lakini ni 
imani kuwa kabila hilo litaendelezwa kupitia tamasha la Urithi Wetu.
Mwenyekiti
 huyo wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Urithi Kitaifa amesema 
"Utalii wa Utamaduni utainuliwa kupitia Urithi festival.
Amewaomba
 Watanzania kushiriki vema kwenye Tamasha hili na kuvaa mavazi ya 
Kitanzania kama vitenge, ngozi, batiki, shuka na mavazi mengine ya asili
 katika maadhimisho haya na ya kila  Mwezi wa tamasha la Urithi.
"Urithi
 festival inatoa fursa kwa watu wote. Tunapenda waje hapa waone ubunifu,
 vitu muhimu na mambo ya ubunifu wa kila aina” Amesema Profesa Mabula.
Ameongeza kuwa, Watu tuheshimu Urithi wetu wa Utamaduni ili kuchochea Utalii wa ndani na nje ya Nchi.
Tamasha
 hilo limepambwa na  vikundi mbalimbali vya ngoma za kiasili, sarakasi, 
nyimbo, Wajasiriamali, vyakula vya kiasili ikiwemo nyama choma za 
porini  kama swala na nyati zilnazouzwa kwa shilingi elfu Nane kwa kilo.
Naye
 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw.
 Richard Mayongela  katika kuunga mkono Tamasha la Urithi Wetu, 
imekabidhi fulana 100 katika hafla hiyo.
Tamasha
 hilo ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka, linaandaliwa na Wizara ya 
Maliasili na Utalii, na lilizinduliwa rasmi Septemba 15 mwaka huu jijini
 Dodoma na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia 
Suluhu Hassan likiwa na lengo la kuongeza idadi ya watalii nchini.
Imeelezwa
 kuwa, baada ya Tamasha hilo kufungwa rasmi jijini Dar-es-Salaam 
litaendelea kufanyika Jijini Arusha kwenye Uwanja wa Sheikh  Amri  
Abeida Karatu, ambako ni njia kuu ya kuingilia katika Hifadhi ya Bonde 
la Ngorongoro na Serengeti kuanzia Oktoba 8  hadi  13.






No comments:
Post a Comment