Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania (TFF) Wakili Revocatus Kuuli amejiuzulu wadhifa huo.
Kuuli
 amefikia hatua hiyo kwa kumuandikia barua Rais wa TFF, Walace Karia 
iliyoeleza kujiuzulu nafasi ya Uenyenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa 
TFF.
Kuuli
 ameeleza sababu  ya kufanya maamuzi hayo ni kutokana na kuingiliwa 
majukumu yake ya kazi na katibu mkuu wa TFF Wilfred Kidao.
Hivi
 karibuni Kuuli alitangaza kuupiga STOP mchakato wa uchaguzi wa klabu ya
 Simba baada ya kubainika ulikuwa na mapungufu kadhaa, na baadaye Kaimu 
Katibu Mkuu, Wilfred Kidao akamjia juu.
Kidao
 alikuja na kumtaka kuandika barua ya maelezo ikimtaka aeleze maamuzi 
hayo ameyatoa wapi huku akipewa siku tatu pekee awasilishe majibu.
Baada
 ya kupewa amri hiyo Kuuli alimjia juu pia Kidao na kueleza kuwa hawezi 
kuingiliwa katika majukumu yake na mpaka imepelekea atangaze maamuzi ya 
kuachia ngazi.






No comments:
Post a Comment