Waziri
 wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo na kiongozi wa Korea kaskazini 
Kim Jong UN wamekubaliana kupanga mkutano wa awamu ya pili kati ya 
Marekani na Korea kaskazini haraka iwezekanavyo, ofisi ya Rais wa Korea 
kusini ilisema Jumapili.
Tangazo
 hilo lilikuja muda mfupi baada ya Pompeo alipowasili Seoul kufuatia 
ziara yake ya siku nne kuelekea Korea kaskazini mahala ambapo alikutana 
na Kim. 
Pompeo
 alisema Marekani na Korea kaskazini walikubaliana kuendeleza mazungumzo
 na kuchagua tarehe maalumu pamoja na mahala ambako mkutano ujao 
utafanyika kulingana na taarifa kutoka ofisi ya Rais wa Korea kusini, 
Moon Jae-In.
Moon
 alimshukuru Pompeo kwa ziara yake na aliwatakia mafanikio mema kwenye 
mkutano ujao kati ya Kim na Rais Donald Trump wa Marekani. 
Viongozi hao wawili walikutana mara ya mwisho mwezi June mwaka 2018 huko Singapore.






No comments:
Post a Comment