Serikali Yayataka Vibali Vya Ujenzi Kutolewa Ndani Ya Siku Tatu

Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatoa vibali vya ujenzi wa nyumba ndani ya siku tatu na kazi hiyo isimamiwe na Maofisa Mipango Miji.

Aidha, imesisitiza kuwa zoezi la urasimishaji katika maeneo yaliyojengwa nyumba kiholela lazima yarasimishwe na zoezi hilo halitakiwi kubomoa nyumba ya mtu yoyote.

Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi wakati akifungua mkutano wa tano wa Bodi ya Wataalamu wa Usajili Mipango Miji unaoendeleo katika jiji la Dodoma.

Lukuvi alisema vibali vya ujenzi wa nyumba katika maeneo mbalimbali lazima vitolewe aidha katika eneo lililopangwa ama lisilo pangwa na cha msingi serikali inachotaka ni kuwa na majengo yaliyo katika mpangilio mzuri na kuongeza kuwa ucheleweshwaji wowote utoaji kibali lazima mhusika afahamishwe sababu za kucheleweshewa kupatiwa kibali.

Kwa mujibu wa Lukuvi lengo la Maofisa Mipango Miji kupewa mamlaka ya kutoa vibali vya ujenzi badala ya wakuu wa idara wa halmashauri husika linatokana na baadhi yake kuongozwa na watu wasiokuwa na taaluma za mipango miji jambo linaloweza kuvuruga upangaji miji bora kwenye maeneo.

Pia ametaka nakala za vibali vya ujenzi vitakavyotolewa na kuhakikisha nakala hizo za vibali zinaenda pia katika ofisi za maafisa watendaji wa mitaa kwa kuwa watendaji hao wanapaswa kufahamu ujenzi unaoendelea katika maeneo yao.

Lukuvi ameitaka Bodi ya Usajili Mipango Miji kuandaa muongozo utakaosaidia watendaji wa mitaa kuwa na ufahamu katika kusimamia mipango ya uendelezaji miji jambo litakalosaidia pia kuepuka   ujenzi holela katika baadhi ya maeneo.

Akigeukia suala la urasimishaji maeneo yasiyopimwa, Lukuvi alisema pamoja na zoezi hilo kufanyika nchi nzima lakini hakuna nyumba itakayovunjwa katika zoezi hilo na kutaka makampuni yote yatakayotaka kufanya kazi ya urasimishaji kutuma maombi yao kupitia ofisi za wilaya na kuacha kuenda moja kwa moja kufanya kazi hiyo kupitia kamati maalum za maeneo husika na kusisitiza kuwa zoezi hilo lazima liratibiwe na Maofisa Mipango Miji.

Katika hatua nyingine, Lukuvi amepiga marufuku upimaji mashamba katika maeneo mbalimbali bila ya kupangwa na kubainisha kuwa serikali haitakubali kadhia hiyo iendelee kushamiri kwani suala hilo linafanya miji kukosa maeneo ya wazi, mashule, masoko na hospitali.

Salfonce Kesi Mtafiti na mwalimu katika Chuo cha Ardhi alisema, kwa sasa mambo mengi ya upangaji miji katika maeneo mbalimbali nchini hayaendi vizuri kutokana na mipango kufanywa na watu wasio na taaluma ya mipango miji.

Alisema, ni lazima suala la mipango miji katika maeneo lianze ndipo mipango mingine ya maendeleo iendelee kama vile huduma za maji, barabara pamoja na huduma nyingine za jamii.

Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili Mipango Miji Profesa Wilbert Kombe alisema bodi yake imeanza kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha taaluma ya Mipango Miji inakuwa na wataalamu wanaozingatia sheria na kuchangia kuwepo miji bora na iliyopangika na kubainisha kuwa mahali popote sura ya miji ndiyo inayotoa taswira ya maisha ya eneo husika.
Share:

Makamu wa Rais: Msichague Viongozi Mazezeta Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa 2019

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Samia Suluhu amewataka wananchi wa Kibaha Mjini Mkoani Pwani ,wajipange kuchagua viongozi wepesi kufuatilia maendeleo na kwenda mbio badala ya kuchagua mazezeta na mananga ,katika uchaguzi unaokuja wa serikali za mitaa- 2019.
 
Akihitimisha ziara yake ya siku sita mkoani hapo katika mkutano wa hadhara ,Mailmoja Samia aliwasihi wasichague watu wazito,wezi na mafisadi bali waweke viongozi watakaojenga Kibaha .
 
“Wanasema mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe ,mimi nikija ninaona kasoro zilizopo nitakwambieni kuna kasoro lakini warekebishaji ni nyinyi na viongozi mtakaowachagua “;:
 
“Mkichagua wazuri wataondosha kasoro zilizopo haraka lakini mkichagua wazito na mananga hapa yatazama tuu chini kunyanyuka hayanyanyuki ,kutembea hayatembei “alisisitiza Samia .
 
Akizungumzia suala la ardhi anasema”:; Wakati napita ,mheshimiwa mkuu wa mkoa alinionyesha eneo kubwa halina kitu chochote nikamwambia mnataka manispaa ,lakini mbona eneo hili mwitu mtupu hakuna kuendelezwa akaniambia linamilikiwa na taasisi fulani “
 
Aidha ,ameitaka wilaya na halmashauri ya Mji huo kukaa chini na taasisi ambazo zimehodhi maeneo bila kuyaendeleza katika kipindi kirefu ili ziweze kuingia ubia  .
 
Awali Mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini ,Silvestry Koka aliomba mji huo upandishwe hadhi na kuwa manispaa kama vigezo vinaruhusu.
 
Alitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni ,usambazaji wa maji kwenda kwa wananchi unasuasua kasi iongezwe kwani mji unakua ila maji hayajawafikia .
 
” Eneo la Tamco-Mapinga zaidi ya miaka mitano wapo wananchi walifanyiwa tathmini lakini hawajalipwa fidia zao ,tunaomba utusaidie wananchi hawa waweze kufaidika na fidia hizo”alielezea Koka.
 
Koka alitaja tatizo jingine ni ucheleweshaji wa nishati ya umeme , kasi ni ndogo kufika kwa baadhi ya maeneo na wawekezaji ,ameomba uwafikie maeneo yaliyo katika miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.
 
Akijibu changamoto hiyo, Naibu waziri wa nishati ,Subira Mgalu alisema , kupitia serikali ipo sheria iliyoanzisha wakala wa nishati ya umeme vijijini lakini maeneo ya miji sheria ile ilikuwa huwezi kufanya miradi ya umeme mijini.
 
“Serikali ya awamu ya tano kwa makusudi mazima iliona miji ifaidike na raslimali zinazopatikana kwenye mfuko wa umeme vijijini na kwa maelekezo yenu tulibuni mradi wa Peri Urban”;alifafanua Subira.
 
Subira alisema ,kiasi cha sh. bilioni 82 zimetengwa kwa ajili ya mradi huo na sasa hatua iliyopo ni kumpata mkandarasi ili mradi uanze kazi .
 
Aliwahakikishia wananchi ambao hawana umeme katika kata ya Mailmoja ,Viziwaziwa,Pichandege ,Pangani, Misugusugu ,Sofu watanufaika na mradi huo .
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ramadhani Maneno, alisema Pwani ipo salama na ushindi ni lazima ,iwe jua iwe mvua uchaguzi ujao wa serikali za mitaa atahakikisha wanashinda
Share:

Waziri Mkuu: Nimeridhishwa na Hatua za Awali za Uwekezaji Mkinga


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea eneo la mradi wa ujenzi wa viwanda 11 katika kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga, ambapo amesema ameridhishwa na hatua za awali za uwekezaji huo.

Katika eneo hilo vinatarajiwa kujengwa viwanda mbalimbali kikiwemo cha saruji cha Hengya, kiwanda cha vioo, kiwanda cha vifaa vya kisasa vya ujenzi, uzalishaji wa umeme kwa kutumia makaa ya mawe.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Oktoba 30, 2018) wakati akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tanga.

Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kulinufaisha Taifa na wananchi wakazi wa wilaya ya Mkinga kwa kuwa kinatarajiwa kuajiri zaidi ya watu 8,000, hivyo amewaomba wananchi hao waendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji hao.

Kuhusu wananchi ambao eneo lao limechukuliwa na wawekezaji na bado hawajalipwa fidia Waziri Mkuu amewataka wawe na subira kwa kuwa wote watalipwa. “Muwekezaji amenihakikishia kwamba atawalipa wananchi wote wanaodai fidia.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuuamewataka watumishi wa umma kutenga siku tatu katika wiki na kuwafuata wananchi waishio maeneo ya vijijini kwa ajili ya kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.

Amesema Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwatumikia wananchi bila ya ubaguzi wa kidini, kisiasa, rangi  na kimapato, hivyo amewataka watumishi hao wafanye kazi kwa bidii.

Awali, Mbunge wa jimbo la Mkinga, Dastan Kitandula ameishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi wa Mkinga baada ya Serikali kufuta hati ya shamba la moa na kuirudisha ardhi hiyo kwa wananchi, pia ameomba ifute hayi za mashamba mengine yaliyotekelezwa katika Tarafa ya Maramba.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, OKTOBA 30, 2018.
Share:

CCM Yasema Mwisho wa Kuwapokea Wanaohamia Toka Vyama Vingine ni Novemba 15....Tazama Hapa Maamuzi ya Kamati Kuu

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimewapitisha makada wake wanne kuwania nafasi ya ubunge katika maeneo yao kufuatia kikao cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kukutana leo jijini Dar es salaam.
 

CCM imewapitisha waliokuwa wabunge wa maeneo hayo kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), waliotangaza kujiunga na chama hicho kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli.

Wabunge hao waliopitishwa ni Pauline Gekui wa jimbo la Babati, James Milya jimbo la Simanjiro, Joseph Mkundi Jimbo la Ukerewe, na Marwa Ryoba ambaye atawania nafasi ya ubunge jimbo la Serengeti.

Aidha Chama hicho kimetaja tarehe 15 novemba kuwa ndio tarehe ya mwisho kwa Chama hicho kuwapokea maombi ya wenye nia ya kujiunga na Chama hicho na kupewa dhamana ya uwakilishi kupitia tiketi ya CCM kwa wabunge na madiwani kutoka vyama vingine.

Aidha taarifa hiyo imesema baada ya tarehe hiyo hakuna kiongozi yeyote atakayepewa nafasi ya kugombea uwakilishi wa Chama hicho katika uchaguzi wa marudio badala yake watakuwa wanachama wa kawaida.
Share:

Dr Mengi Kuanzisha Kiwanda Cha Kutengeneza Simu za SmartPhone Hapa Nchini....Simu Zitakuwa na Uwezo wa Kukaa cha Chaji Wiki 2

Mfanyabiashara maarufu Tanzania, Dk. Regnald Mengi ametambulisha ujio wa kampuni yake mpya ambayo itakuwa ni ya kwanza Tanzania kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali za Kielektroniki, ikiwa ni pamoja na simu za mikononi, simu janja (Smartphones), computers, Ipads, music bluetooth speakers, headphones, earphones .

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Dk Mengi amesema simu ambazo zitatengenezwa zitakuwa zinakaa na charge kwa zaidi ya wiki moja zikiwa ni maalumu kwa mazingira yenye matatizo ya umeme hasa vijijini pia aina hizo za simu zitatumika kama power Bank kucharge simu zingine.

Aidha ameeleza kuwa wanatarajia kutoa ajira zaidi ya 2000 rasmi na zisizo rasmi na kampuni itatoa kipaumbele katika kuajiri wenye ulemavu, wenye sifa stahiki
 
 
Share:

Mwenyekiti Wa CCM Rais Magufuli Aongoza Kikao Cha Kamati Kuu Ya Chama Hicho Jijini Dar Es Salaam


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ofisi ndogo za chama hicho mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam leo Okotoba 30, 2018
 
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu Mwenyekiti wake (Bara) Ndg. Philip Mangula na Katibu Mkuu Dkt. Bashiru Ally, baada ya kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ofisi ndogo za chama hicho mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam leo Okotoba 30, 2018
 
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan baada ya kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ofisi ndogo za chama hicho mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam leo Okotoba 30, 2018. 
 
Kati yao ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndg. Philip Mangula na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai
 
Share:

Polisi,tra Kilimanjaro Wanasa Kiwanda Feki Cha Kutengeneza Pombe Kali.

JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamefanikiwa kukamata kiwanda  cha kutengeneza Pombe kali ambacho kimekuwa kikizalisha bidhaa hiyo bila ya usajili.

Moja ya dira za serikali ya awamu ya tano ni kufikia uchumi wa kati kupitia Viwanda ,hata hivyo baadhi ya wafanyabiahara wanatafsiri Dira hii tofauti kwa kuamua kuanzisha Viwanda bila ya kufuata matakwa ya Sheria na taratibu za nchi.

Hali hii imejidhihirisha mkoani Kilimanjaro katika mji mdogo wa Himo baada ya Polisi,TRA na TFDA kubaini uwepo wa kiwanda bandia kinachozalisha Pombe kali .

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamisi Issah amesema jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na idara nyingine za serikali kuhakikisha kodi ya serikali inapatikana pamoja na kuhakiki ubora wa bidhaa kwa ajili ya afya ya watumiaji.

Zoezi la kubaini uwepo wa viwanda bandia katka mkoa wa Kilimanjaro ambapo katika siku za karibuni viwanda vilivyogundulika ni vile vinavyotengeneza Pombe za kienyeji na Pombe kali ,baadhi  vikiwa katika wilaya ya Rombo.
Share:

Shahidi adai Mshahara na Posho za mhasibu Takukuru Ilikuwa Sh 334,175,332.05.

Ofisa  Uchunguzi Mwandamizi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Naza Alawi (43), amedai mahakamani kwamba  aliyekuwa  Mhasibu Mkuu wa Takukuru, Godfrey Gugai, alifukuzwa kazi baada ya kukutwa na hatia ya kukosa uaminifu.

Kipato cha mshtakiwa huyo cha mshahara na posho katika kipindi chote cha ajira kilikuwa   Sh 334,175,332.05.

Shahidi huyo alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Akingozwa na Wakili wa Serikali Vitalis Peter, shahidi alidai majukumu yake kusimamia dawati la mishahara, kuandaa malipo, kulipa kodi mbalimbali na kutunza kumbukumbu ya daftari la watumishi waliokopa.

“Gugai alianza kazi Juni mwaka 2001 hadi Julai mwaka 2016 utumishi wake ulipokoma baada ya kufukuzwa kwa kukosa uaminifu.

“Alikutwa na mali ambazo hakuzitolea tamko kwenye tamko la mali, nilipewa maelekezo na mhasibu ya kuchambua mishahara ya Gugai kuanzia alipoanza kazi hadi alipofukuzwa, “alidai.

Alawi alidai mshahara wa Gugai alipoanza kazi Julai mwaka 2001 ulikuwa Sh 152,630, Februari mwaka 2004 ulipanda na kufikia Sh 191,822.15 ,hadi anafukuzwa kazi mshahara wake ulikuwa Sh 4,417,838.

Anadai posho za mazingira magumu Julai mwaka 2001, alikuwa analipwa Sh 45,000, Machi mwaka 2008 alilipwa Sh 341,784 na mpaka anafukuzwa posho hiyo alikuwa analipwa Sh 1,362,800.

Shahidi alidai posho ya matibabu alilipwa Sh 150,000 kuanzia Agosti mwaka 2006 hadi Juni mwaka 2003 na posho ya nyumba ilikuwa Sh 92,858.40 Julai 2007 na Mei mwaka 2009 ilipanda na kuwa Sh 142,450.

“Kwa kipindi chote cha ajira Gugai alilipwa   mshahara wa Sh 218,916,859.65, posho ya mazingira magumu  Sh 99,944,099.50, posho ya matibabu Sh 12,450,000 na posho ya nyumba j Sh 2,864,372.90.

“Jumla ya kipato chote cha Gugai katika kipindi chake cha ajira ni Sh 334,175,332.05,”alidai Alawi.

Shahidi huyo pia alichambua mshahara na posho za mke wa Gugai, Lina Francis, aliandikia ripoti ambayo alitaka kuitoa mahakamani kama kielelezo.

Wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa alipinga kuwasilishwa   ripoti hiyo akidai kwamba muhusika hakuwapo  mahakamani.

Baada ya hoja hiyo mahakama iliahirisha kesi hadi leo kwa ajili ya kuendelea na ushahidi baada ya kujiridhisha kuhusu sheria inasemaje katika mazingira hayo.

Mbali na Gugai, washtakiwa wengine  ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasin Katera.

Katika kesi ya msingi, Gugai na mwenzake wanakabiliwa na makosa 43, kati ya hayo 19 ni ya kughushi, 23 ni utakatishaji fedha na moja ni kumiliki mali zilizozidi kipato halali.

Gugai anakabiliwa na shitaka la kumiliki mali kinyume na kipato chake, ambako alitenda kosa hilo kati ya January 2005 na Desemba 2015.

Inadaiwa   akiwa  Dar es Salaam kama mwajiriwa wa Takukuru alikuwa akimiliki mali za zaidi ya Sh bilioni 3.6 ambazo hazilingani na kipato chake cha awali na cha sasa huku akishindwa kuzitolea maelezo.
Share:

RC Makonda: Nimepokea meseji 5763 kati ya hizo kuna majina 100 ya mashoga wa Dar

Ikiwa ni siku moja toka Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda atangaze kampeni ya kuanza kuwakamata mashoga pamoja na malaya ambao wanajiuza kupitia mitandao ya kijamii, ameanza kupata mrejesho.

Hatua hiyo imekuja baada ya msanii wa muziki, Amber Rutty kuachia video chafu mtandaoni hali ambayo ilimfanya mkuu huyo kutoa tamko la kutaka akamatwe.

RC Makonda alisema kwa tukio ambalo amelifanya msichana huyo anapaswa kufungwa jela, kwani ni ukiukwaji wa sheria za nchi huku akiwataka Wanadar es salaam kumtumia majina ya mashoga pamoja na watu ambao wanafanya biashara ya ngono mtandaoni.

“Nimepokea msg zaidi 5,763 na majina ya Mashoga zaidi ya 100 hii inaonyesha Wana DSM hawataki laana ya mashonga. Naendelea kupokea majina ya Mashoga,” amesema RC Makonda kupitia taarifa aliyoitoa siku ya leo.

Mkuu huyo amesema msako mkali wa kamata kamata ya mashoga na watu wanaojiuza utaanza wiki ijayo kwani kwa sasa anakiandaa kikosi kazi pamoja na kupokea baadhi ya majina.
Share:

Waganga wafawidhi watakiwa kujadili sababu ya vifo vinavyotokea kwenye hospitali zao

Waganga  wafawidhi wametakiwa   kujadili sababu ya vifo vinavyotokea kwenye hospitali zao ili kuzifanyia kazi changamoto hizo na kurudisha taarifa Wizara ya Afya.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Wizara ya Afya, Dk. Otilia Gowelle, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa waganga wafawidhi nchini,  Dodoma jana.

“Waganga wafawidhi mnatakiwa kukaa vikao vya utabibu kujadili tiba pamoja na kujadili kifo cha kila mgonjwa  kujua changamoto iliyotokea na kuipatia ufumbuzi na kuandikia taarifa   kuondokana na vifo hasa vinavyotokana na uzazi,” alisema Dk. Gowelle.

Aliwataka wataalamu wa tiba kuzingatia vikao vya tiba na kufanyia kazi changamoto au maboresho ili kuzitolea taarifa na kuzitatua pamoja na kushirikisha wadau wengine.

Dk. Gowelle aliwataka pia waganga wafawidhi kuweka mifumo ya ufuatiliaji wagonjwa   na kupokea malalamiko  katika hospitali zao   kufanya maboresho ya huduma za afya wanazozitoa na kuchukua hatua zinazostahili.

“Kupitia kikao hiki, nawataka mkae kama timu na kuandaa mipango kazi ya kuanza kushughulikia kwa ukamilifu yale yote yaliyobainika katika taarifa hiyo.

“Lengo ni kuondokana na kero wanazokabiliana nazo wananchi wanapokuja kupata huduma katika hospitali zenu,” alisema Dk. Gowelle.
Share:

Angela Merkel atangaza kuachia ngazi 2021


Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel ametangaza kuwa hatagombea tena uongozi wa chama chake cha Christian Democratic Union -CDU, na kwamba muhula wa sasa wa ukansela ambao ni wa nne madarakani utakuwa wa mwisho.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama chake jijini Berlin, ambapo amesema kuwa muda umewadia wa kufungua ukurasa mpya.

Merkel mwenye umri wa miaka 64 amekuwa mwenyekiti wa chama cha CDU tangu mwaka 2000, na Kansela wa Ujerumani tangu mwaka 2005 ambapo katika kipindi cha miaka 13 kama Kansela, amekuwa pia mwanasiasa maarufu barani Ulaya.

Aidha, Merkel amegusia mivutano ya ndani ya vyama vinavyounda mseto wa serikali anayoiongoza, ambayo imesababisha mzozo baada ya mwingine, na kuhitimisha kwamba taswira inayotoka katika serikali hiyo haikubaliki.

“Kwa uamuzi huu najaribu kuchangia katika kuiwezesha serikali ya Ujerumani kujikita katika juhudi za uongozi bora, suala ambalo wananchi wamekuwa wakidai, kitu ambacho ni haki yao, hatua hii vile vile inakwenda sambamba na azma ya serikali ya Ujerumani kufanya tathmini ya nusu muhula, kuhusu ilivyotekeleza majukumu yake, kama ilivyokubaliwa na vyama vya CDU, CSU na SPD katika mkataba wa kuunda serikali ya mseto.” amesema Merkel

Hata hivyo, mwanasiasa huyo wa Ujerumani ambaye alikuwa akichukuliwa kama mwanamke mwenye nguvu zaidi duniani, na mwenye kauli ya mwisho katika Umoja wa Ulaya, alianza kupoteza ushawishi baada ya uamuzi wake wa kuruhusu wakimbizi zaidi ya milioni moja kuingia nchini Ujerumani mwaka 2015.
Share:

Tanzania Yashikilia Msimamo Wake wa Kutosaini Mkataba wa EPA


Waziri  wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, ameongoza ujumbe wa Tanzania ulioshiriki mkutano  wa pamoja wa 16 wa mawaziri wa biashara wa nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (ACP) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika  Brussels.  Ubelgiji.

Kwenye mkutano huo Tanzania ilisisitiza azma ya kutosaini mkataba wa EPA.

Mbali na mkutano huo, Profesa Kabudi alishiriki mkutano wa 21 wa Kamati ya Mawaziri wa Biashara wa ACP.

Taarifa   iliyotolewa jana, ilisema mikutano hiyo miwili ilitanguliwa na mkutano wa makatibu wakuu wa nchi za ACP wanaosimamia masuala ya biashara.

Ilisema katika mkutano huo, Tanzania ilisema mkataba wa EPA hauwezi kuwa nguzo au chachu ya maendeleo  kama ilivyo katika malengo yake kwa kuwa hautoi fursa kwa nchi za ACP kukuza sekta ya viwanda na biashara.

Ilisema badala yake mkataba huo una sura ya misaada kutoka EU kwenda ACP na umelenga nchi za ACP kuwa soko kuu la bidhaa za EU.

Taarifa hiyo ilisema mkataba huo una vikwazo vingi visivyo vya ushuru ambavyo husababisha nchi za ACP zishindwe kufanya biashara ya bidhaa na huduma na nchi mbalimbali za EU.

“Tanzania ilirejea msimamo wake wa awali wa kutosaini mkataba wa EPA hadi hapo utakapoboreshwa na kuwa na sura ya ushirikiano wa maendeleo ya uchumi.

“Baada ya Tanzania kutangaza msimamo wake, baadhi ya nchi nyingine za ACP ziliunga mkono hoja hii na kuhamasisha nchi nyingine zaidi za ACP zichukue msimamo wa Tanzania,” ilisema taarifa hiyo.

Ilisema katika mikutano hiyo   Profesa Kabudi aliongozana na Naibu Katibu Mkuu, Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dk. Edwin Mhede na wataalamu wengine waandamizi kutoka Wizara ya Viwanda, Viashara na Uwekezaji, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania jijini Brussels.

Tanzania ni miongoni mwa wanachama wa Nchi za  Afrika, Caribbean na Pacific (ACP)   tangu mwaka 1975. Nchi hizo za ACP zimekuwa na majadiliano na Umoja ya Ulaya (European Union – EU) kwa lengo na kukuza ushirikiano miongoni mwao.
Share:

Uteuzi Mwingine Tena Uliofanywa Na Rais Magufuli Leo October 30


Share:

RC Makonda Afunguka Tena Sakata la Video Chafu za Amber Rutty


Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda amefunguka tena kuhusiana na video chafu za mrembo Amber Rutty na mpenzi wake lakini pia kuhusiana na ongezeko la mashoga katika jiji la Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari jana October 29, 2018, RC Makonda alisema kuwa Amber Rutty na mpenzi  wake bado  wapo lupango  wakati wanasubiriwa kupandishwa kizimbani na kuweka wazi kuwa adhabu yao ni kifungo cha  maisha jela au miaka 30 kama itatbitika wanafanya kinyume na maumbile.

"Tayari yule binti anayeitwa Amber Rutty pamoja na bwana yake wapo chini ya polisi tangu kipindi kile nilivyotoa maelekezo na niseme kuwa kosa lile liko wazi na sheria inasema ni aidha kifungo cha maisha au miaka 30, hiyo yote ni kuonyesha ni jinsi gani serikali isivyopendezwa na mienendo inayomomonyoa maadili ya taifa letu”. Alisema Makonda

Lakini pia RC Makonda alitangaza vita na mashoga wote ambao wanajihusisha na shughuli za kufanya mapenzi kinyume na maumbile;

"Naomba nitoe fursa hii kwa wakazi wa Dar es Salaam, namba yangu ya simu inafahamika .Nimepata taarifa kwamba kuna mashoga wengi sana kwenye mkoa wetu na mashoga hawa ndio kazi yao wanajinadi kwenye mitandao ya kijamii, kwa hiyo nawaambia wananchi kama kuna shoga yoyote unamfahamu leo mpaka jumapili napokea taarifa zao”.
Share:

IGP Sirro Akutana Na Kikosi Maalum Kinachopambana Na Uhalifu Wilayani Biharamulo

 

Askari wa kikosi maalum kinachopambana na matukio ya uhalifu na wahalifu kama wanavyoonekana Pichani wakitekeleza majukumu yao katika eneo la Midaho wilayani Biharamulo mkoani Kagera jana 29/10/2018. Picha na Jeshi la Polisi.
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na askari wa kikosi maalum cha kupambana na matukio ya uhalifu na wahalifu katika eneo la Midaho wilayani Biharamulo mkoani Kagera jana 29/10/2018 wakati akiwa safarini  kuelekea wilaya ya Ngara mkoani humo kwa ziara ya kikazi. Picha na Jeshi la Polisi. 
Share:

Waziri wa Kilimo: Hatuwezi Kuendelea Kuagiza Sukari Wakati Tuna Uwezo Wa Kufanikisha Uzalishaji

Serikali imeipa changamoto Bodi ya sukari nchini kutekeleza majukumu yake kwa weledi ikiwa ni pamoja na kusisitiza kuhuisha uzalishaji wa sukari kwa wingi ili kuondokana na uagizaji wa sukari kutoka nje ya nchi.

Kampuni mbalimbali za uzalishaji wa sukari nchini zimeitikia wito wa Serikali wa kuongeza uzalishaji wa sukari ili nchi iweze kujitegemea kwa bidhaa hiyo pendwa kwa matumizi ya nyumbani na viwandani na ziada jambo litalopelekea Bodi ya sukari kusimamia majukumu yake ipasavyo ili kuondokana na uagizaji wa sukari nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo jumatatu tarehe 29 Octoba 2018 na Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb)  wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi ya Sukari Tanzania (SBT) hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Mjini Dodoma.

Waziri Tizeba amemtaka Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari nchini Bi Mwamini Juma Malemi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Prof Kenneth Michael Kitundu Bengesi Kudhibiti sukari inayoingia nchini pasina utaratibu huku akiwataka kusimamia kwa weledi ufanisi katika uongezaji wa uzalishaji wa sukari nchini.

Aidha, Dkt Tizeba alisema kuwa ufungashaji wa sukari kwenye ujazo wowote ule kwa kutumia vifungashio vya aina yoyote kama vile mifuko yenye nembo ya SUPER FINE lazima uzingatie Sheria ya Sukari Namba 26 ya Mwaka 2001 ambayo inazuia ufungashaji wa sukari bila kupata idhini ya Bodi ya Sukari Tanzania.

Alisema kuwa kwa mujibu wa Sheria hiyo ni marufuku kufungasha au kuuza sukari nyeupe kwa kuwa sukari hiyo ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani kama malighafi na sio kwa ajili ya matumizi ya kawaida majumbani.

Alisisitiza kuwa Mtu yeyote atakayebainika kuvunja Sheria hiyo ya Sukari, atawajibika kulipa faini ya kiasi cha fedha kisichopungua Shilingi Milioni Kumi (10,000,000) au kifungo cha miaka mitatu (3) jela au vyote kwa pamoja.

“Kuna watu wanaolipa kodi ili wazalishe sukari lakini inapoingia sukari ambayo imepenya kinyemela hata ulinganifu wa soko madukani unakuwa mdogo kwa kuwa wanaoingiza bila utaratibu wanauza kwa kiasi cha chini kwa kuwa hawana uchungu wa kulipa kodi”

“Na hili sio jambo la hiara Bodi ni lazima isimame kidete kubaini mianya yote ya wafanyabiashara wanaoingiza sukari bila utaratibu” Alikaririwa Dkt Tizeba

Kuhusu sukari ya viwandani (Industial Sugar) Dkt Tizeba alisema kuwa, wafanyabiashara wamekuwa wakiomba kiwango kikubwa cha kibali cha uagizaji wa sukari lakini serikali ikihakiki kupitia kodi waliyolipa inakuwa haifanani na kiasi kilichoagizwa.
Share:

Waziri aomba radhi kuvuja kwa picha zake za ngono


Waziri wa Mambo ya Ndani wa Afrika ya Kusini , Malusi Gigaba ameomba radhi mara baada ya video yake ya ngono kuvuja mtandaoni.

Waziri Gigaba amesema kuwa video hiyo ilirekodiwa kwa ajili ya matumizi binafsi ya yeye na mke wake ambapo video hizo zilivuja mara baada ya simu yake kudukuliwa na wahalifu wa mtandaoni mwaka jana.

Amesema video hiyo ilianza kusambaa mara baada ya wahalifu hao wa mtandaoni kumtaka atoe kiasi cha fedha alipochaguliwa kuwa Waziri wa fedha mwaka 2017.

Tayari taarifa juu ya wahalifu hawa zipo mikononi mwa sheria, hivyo uchunguzi wa kina unaendelea kufanyika.

Gigaba ameomba radhi kwa umma pamoja na familia yake hasa watoto wake, mama yake na mama mkwe wake kwa machungu na aibu kali aliyoisababisha kutokana na kusambaa kwa video yake akiwa faragha.
“Mke wagu na mimi tumesikitishwa na video hiyo ya ngono ambayo tulikuwa tuione sisi wawili tu kwani mawasiliano yangu ya simu yalidukuliwa mnamo 2016/17 na sasa inazungushwa miongoni mwa wanasiasa.

“Nachukua fursa hii kuomba msamaha kwa watu wengine wa familia yangu, hususan wanangu, mama yangu na wakwe zangu na wananchi wa Afrika Kusini kwa matatizo yatokanayo na jambo hili,” amesema Gigaba.

Katika video hiyo ya sekunde 13, Gigaba yuko peke yake akichezea uume wake kwa mkono na akisema: “Fikiria hiki kingekuwa mdomoni mwako.”
Share:

TCRA Yatoa ONYO Kwa Wanaosambaza Picha na Video za Ngono Mitandaoni


Share:

Rais Magufuli amteua Prof. Humphrey Mushi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ushindani- FCC






Share:

Mastaa Mbalimbali Wamlilia Producer Pancho Latino


Wadau mbalimbali wa sanaa na burudani wameanza kutoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu mzito wa  producer Pancho Latino uliotokea leo October 9,2018 katika kisiwa cha Mbudya Dar es Salaam.
==>>Hawa ndio baadhi ya mastaa walioguswa na taarifa hizo na kuziandika kupitia kurasa zao za instagram

“Pancho Pancho Pancho nimeumia sana sina mfano wa maumivu niliyopata dah! Pumzika kwa Amani na Asante kwa mchango wako mkubwa katika Muziki Wetu…Bwana alitoa na Bwana Ametwaa jina lake lihimidiwe” -Joh Makini

“Eh Mungu … 😭 Rest Easy Young Legend. Thankyou for everything you taught me, you raised me #BHitz you will live forever in the music 🙏🏾. Poleni Sana kwa familia nzima ya #BHitz #LatinoMafia@hermyb pigo kubwa kwenye tasnia ya muziki.” -Vanessa Mdee

“Rest In Power Latino Mafia!!!! 😔 I am Sad!! -Bdozen

“Doh..Upumzike kwa amani @pancholatino ..kazi ya Mungu na safari yetu ni moja..nimesikitika mno” -Mwana FA

“Daaah!!! Upumzike kwa Amani, sidhani kama ulikuwa umemaliza ulichokuwa nacho kichwani. Mapema sana, ila kazi ya Mungu haina makosa #RIP“-Marcochali

“Kutokana na msiba uliotufika hivi punde wa kuondokewa na producer Genius PANCHO LATINO kutoka B’HITS…Hatutaweza kuachia VIDEO Yetu ya#USHINDITENA kwa Leo…SO SAD Kwa kweli R.I.P PANCHO LATINO #RIP#genius#mafia #weusii“-Lordeyesmweusi
 
 
 
 
 
Share:

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive