WAZIRI
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amefanya ziara ya kushtukiza 
katika Kituo cha Polisi Katoro mkoani Geita  na kuwahoji watuhumiwa wa 
makosa mbalimbali waliokuwepo katika mahabusu kituoni hapo.
Lugola
 ambaye alikua safarini kuelekea Mkoani Kigoma kwa ziara yake ya kikazi,
 ghafla aliibukia katika kituo hicho akitaka kujua utendaji kazi wa 
polisi pamoja na makosa mbalimbali wanayowakabili watuhumiwa waliopo 
katika mahabusu hiyo na pia kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili 
askari wa kituo hicho.
Lugola
 aliowasili kituoni hapo jana mchana na akaelekea moja kwa moja mahabusu
 na akaomba kitabu cha taarifa ya makosa mbalimbali yaliyoripotiwa 
kituoni hapo, na akamuelekeza askari wa zamu awapange foleni watuhumiwa 
hao ili aweze kuwahoji makosa yao na pia Mkuu wa Kituo cha polisi hicho,
 aweze kufafanua makosa yao.
Baada
 ya watuhumiwa hao, Lugola licha ya kuwapongeza polisi wa kituo hicho 
kwa kufanya kazi vizuri, pia alimtaka Mkuu wa Kituo hicho, Steven Kimaro
 kua makini na utendaji wake na kuwafuatilia kwa umakini utendaji kazi 
wa askari wake kwasababu yeye ndio kiongozi wa kituo hicho.
“Sipendi
 wananchi waonewe, haki itendeke na si kila kosa lazima mtuhumiwa awekwe
 mahabusu, tumieni busara umakini ili tuweze kutenda haki na pia nataka 
jeshi hili liwe na picha nzuri zaidi kwa jamii,” alisema Lugola.
Pia
 alifafanua kua, hataki kusikia askari polisi anatuhumiwa kwa rushwa au 
kunyanyasa wananchi, na endapo taarifa hizo zitamfikia basi atahakikisha
 askari huyo anachukulia hatua za kisheria.
Aidha,
 Waziri Lugola alitaka polisi wa usalama barabarani kufuata sheria na 
pia si kila kosa lazima mwenye gari kuandikiwa risiti ya malipo, makosa 
mengine watoe elimu zaidi kwa madereva hao ili taifa liweze kusonga 
mbele.
Lugola
 Septemba 25 anatarajia kuanza ziara yake ya kutembelea mikoa yote 
nchini, ambapo ataanza ziara katika Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma 
ambapo atazungumza na askari na maafisa polisi, watumishi wa taasisi 
zilizopo katika wizara yake na baadaye atafanya mkutano wa hadhara kwa 
kuzungumza na wananchi pamoja na kusikiliza kero zao mjini humo.






No comments:
Post a Comment