
Mahakama
 ya Hakimu Mfawidhi mkoa wa Iringa  imefunga kusikiliza ushahidi wa  
shauri linalomkabili mwenyekiti wa mtandao wa wanafunzi Abdul Nondo 
baada ya kusikiliza mashahidi wawili wa upande wa utetezi, ambapo 
imepanga Oktoba 2 kutaja siku ya kutoa hukumu ya kesi hiyo.
Kabla
 ya kufunga ushahidi huo Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya mkoa Iringa Liad
 Chamshama amesikiliza mashahidi wawili wa upande wa utetezi ambapo 
shahidi wa kwanza ni  Abdul Nondo  na shahidi wa pili ni  Alphonce 
Lusako.
Akitoa
 ushahidi mbele ya Hakimu  jana Abdul Nondo akiongozwa na wakili wake 
Jebra Kambole, Nondo amedai kuwa alitekwa na watu wasiojulikana karibu 
na geti la chuo cha maji ubungo majira ya  saa tano Usiku, siku ya 
tarehe 6 Machi 2018, kwa kuvamiwa na kutupwa siti ya nyuma ndani ya 
gari.
Nondo
 amesema  watu hao walikuwa wakimhoji kwanini anatumiwa na wanasiasa 
kiasi cha kuvuruga amani na walimtuhumu kuwa anatumiwa na Mwenyekiti wa 
Chadema Freeman Mbowe, Zitto Kabwe na Hellen Kijo Bisimba (aliyekuwa 
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu-LHRC) pamoja na 
kumshutumu kuwa yeye ni wakala wa Mange Kimambi katika kuandaa 
maandamano ya wanafunzi lakini amekana tuhuma hizo. 
Kwa
 upande wake shahidi wa pili Alphoce Lusako ambaye ni kiongozi mwezake 
katika shirika la TSNP ameiambia  mahakama kuwa baada ya kupata taarifa 
kutoka  kwa Paul Kinabo kuwa amepokea ujumbe kwa njia ya simu  kutoka 
kwa Nondo kuwa yupo hatarini  na ndipo wakatoa taarifa kwa uongozi wa 
chuo na askari wasaidizi wa chuo na kupewa RB.
Mtuhumiwa
 Abdul Nondo alifikishwa  Mahakamani Machi 21, 2018 na kusomewa 
mashitaka yake ambayo yote aliyakana kuhusika nayo hivyo Oktoba 2 mwaka 
huu Mahakama itarejea tena kwa ajili ya kutaja siku ya hukumu.






No comments:
Post a Comment