WAFANYABIASHARA WA SANGO WILAYANI KAHAMA WAIOMBA HALMASHAURI KUREKEBISHA MIUNDOMBINU YA SOKO HILO


Na Leah Samson 
KAHAMA

Wafanyabiashara katika eneo la Fantom Mjini KAHAMA wameiomba Halmashauri ya Mji huo kuboresha miundombinu ya soko la Sango kabla ya kuwahamishia katika soko hilo ili kuwawezesha kufanya biashara vizuri na usalama wa mali zao.

Hayo yamesemwa jana na Mwenyekiti wa Wafanyabishara katika eneo hilo, RASHID ATHUMAN, na ABASI SHABANI ambaye ni mfanyabiashara walipokua wakizungumza na kahama FM baada ya kupokea agizo la kuhamia katika Soko la Sango.

Kwa upande wake afisa mtendaji wa eneo hilo, INNOCENT KAPELE amesema ofisi Halmashauri inaendelea na taratibu ya kurekebisha miundombinu ya soko hilo ili kuwa na miundombinu rafiki ikiwa ni pamoja na kudhibiti maji yasiingie.

Amesema ni vyema wafanyabiashara hao wahame katika eneo hilo kwani mazingira si salama kwa kuwa wapo barabarani na hakuna vyoo wakati serikali ikiendelea kurekebisha eneo la Sango.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive