Tume Iliyoteuliwa na Waziri Mkuu Kufanya Uchunguzi Ajali ya MV Nyerere....Itaongozwa na Jenerali mstaafu, George Waitara

 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza tume ya kuchunguza ajali ya Kivuko cha Mv Nyerere, kilichozama Septemba 20 mwaka huu, Ukerewe jijini Mwanza na kusababisha vifo vya watu 224.

Majaliwa ameitangaza tume hiyo ya wajumbe saba itakayoongozwa na Jenerali mstaafu, George Waitara leo Jumatatu Septemba 24, katika Kijiji cha Bwisya, wilayani Ukerewe alipokwenda kushuhudia shughuli ya kunasua miili iliyobaki katika kivuko hicho.

Amesema tume hiyo itaanza kazi mara moja na itafanya kazi kwa muda wa mwezi mmoja.

Aidha, Waziri Mkuu amewataja baadhi ya wajumbe watakaokuwa katika tume hiyo ambao ni Mbunge wa Ukerewe,  Joseph Mkundi, aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Temesa, Mhandisi Celina Magessa na Wakili Julius kalolo ambaye atasaidia mapitio ya sheria na mfumo mzima wa uendeshaji wa vivuko.

“Lakini yumo pia Katibu Mkuu wa UWT, Queen Mlozi kwa ajili ya kusimamia stahili na kina mama, aliyekuwa Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, Bashiru Hussein kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia maafa .Wajumbe hao wanaanza kazi mara moja, waje niwape hadidu za rejea,” amesema Waziri Mkuu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive