Serikali
 wilayani Nkasi mkoani Rukwa, imeagiza kukamatwa kwa wazazi wa 
mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Mkinga aliyepata 
ujauzito kwa kosa la kuandaa mpango wa kumuoza mwanafunzi huyo.
Agizo
 hilo lilitolewa jana na Mkuu wa Wilaya hiyo, Said Mtanda, wakati 
akikabidhi pikipiki 28 zenye thamani ya Sh. milioni 98 zilizotolewa na 
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, kwa kushirikiana na 
Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).
Fedha hizo zilitolewa kwa ajili ya mpango wa kukuza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu kwa waratibu kata wa wilaya hiyo.
Alisema
 katika kijiji cha Mkinga kuna mwanafunzi wa darasa la tatu amepata 
ujauzito na wazazi wake walikuwa wanaandaa mkakati wa kumuozesha, lakini
 walishindwa baada ya Mwalimu Mkuu wa shule hiyo kuingilia kati na 
kuvuruga mpango huo.
"Naagiza
 wazazi wote wa mwanafunzi huyo wakamatwe mara moja, mwanafunzi huyo 
pamoja na aliyempa mimba wafikishwe katika vyombo vya dola, ili sheria 
ichukue mkondo wake na ninyi waratibu elimu kata tambueni mna jukumu 
kubwa la kuhakikisha mimba hizi zinakwisha, " alisema.
Mtanda
 alisema hali hiyo inaonyesha kuwa bado tatizo la mimba ni kubwa kwa 
sababu katika mwezi uliopita jumla ya wanafunzi 27 walipata ujauzito, 
hivyo bado kuna kazi kubwa ya kufanya.
Kwa
 upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Misana Kwangula, 
alisema lengo la serikali kuwapatia pikipiki hizo ni kuwawezesha 
kutembelea shule zilizopo katika kata zao kwa kuwa walikuwa wanalalamika
 kuwa hawana vitendea kazi vya kuwawezesha kufanya ukaguzi katika shule 
wanazozisimamia.






No comments:
Post a Comment