
Mfanyabiashara,
 Masse Uledi (41), amekiri kumiliki simu tisa na laini nane zilizotumika
 kujipatia pesa kwa udanganyifu Sh. milioni 3.6 kama dhamana ya mkopo 
kutoka Focus Vikoba-na kutumia majina ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, 
Salma Kikwete, Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi na Mchungaji Getruda 
Rwakatare.
Uledi
 alikiri madai hayo jana aliposomewa maelezo ya awali katika Mahakama ya
 Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.Maelezo hayo yalisomwa mbele 
ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.
Wakili
 wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita, alidai 2017, mshtakiwa alifungua
 kurasa katika mtandao wa kijamii wa Facebook kwa majina manne tofauti 
akidanganya yanatoa mkopo kupitia Focus Vikoba.
Ilidaiwa
 katika kurasa hizo mshtakiwa alitangaza wanaohitaji mkopo kupitia 
taasisi hiyo, wawasiliane kwa namba za simu, 0759142712, 0714230840 na 
0657076983 ili kupata mkopo.
Ilidaiwa
 kuwa Joyce Chitumbi alipiga simu kuomba mkopo wa Sh. milioni 10, na 
Septemba 9, 2017, alitakiwa kutoa Sh. 840,000 kama dhamana ya mkopo huo.
Upande
 wa Jamhuri uliendelea kudai kuwa Daniel Dangi alitoa dhamana ya Sh. 
600,000 na Sh. 200,000 kwa nyakati mbili tofauti kama dhamana ya mkopo 
wa Sh. milioni mbili.
Mwingine
 anayedaiwa kutapeliwa ni Lucas Kiula, ambaye alitoa ya Sh. 2,160,000 
kama dhamana ya mkopo wa Sh. milioni 10, baada ya kudanganya taasisi 
hiyo iko chini ya Mchungaji Rwakatare wakati akijua si kweli.
Jamhuri ilidai mshtakiwa baada ya kujipatia fedha hizo alizima simu na namba nyingine alipopigiwa hakupokea.
Taarifa
 zilifikishwa Kituo Kikuu cha Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam na 
walifanya uchunguzi wa kimtandao na kubaini mshtakiwa anaishi Kitunda.
Ilidaiwa
 baada ya uchunguzi, Polisi walifanikiwa kufika nyumbani kwake na baada 
ya upekuzi walifanikiwa kumkamata na simu za mkononi nane na laini za 
simu tisa zilizotumika kwenye kurasa za facebook kwa majina ya Rais 
Kikwete, Mama Salma, Mengi na Mchungaji Rwakatare.
Mshtakiwa
 aliposomewa maelezo ya awali, alikiri majina na anuani yake, alikiri 
kumiliki simu na laini hizo kwamba ni mali ya marehemu mumewe.
Katika
 kesi ya msingi ilidaiwa kati ya Septemba 28 na Novemba, 2017 mshtakiwa 
alijipatia Sh. 3,600,000 kama dhamana ya kutoa mkopo wa jumla ya Sh. 
milioni 22 kutoka kwa watu tofauti huku akijua si kweli.
Awali,
 aliposomewa mashtaka hayo alikana na yuko nje kwa dhamana. Kesi 
itaendelea kwa kusikilizwa ushahidi wa Jamhuri Oktoba 11, mwaka huu.






No comments:
Post a Comment