KCB Bank wachangia Mil 125 maafa ya ajali ya Mv Nyerere

Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti na Wafanyakazi wa KCB Bank Group, wameungana na waombolezaji wa msiba uliotokana na kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere kwa kuchangia kiasi cha fedha taslim shilingi 125,000,000/=

Akikabidhi msaada huo wa fedha Mkurugenzi wa Bodi ya KCB, Zuhura Muro, alieleza kuwa wameguswa na maafa hayo na hivyo wanaahidi kuungana na serikali kadri wanavyoweza.

"Tunajua hatuwezi kumaliza shida au mahitaji ya waathirika hawa, hivyo tunapenda kuhamasisha taasisi nyingine zinazoguswa  kama sisi kutoa misaada yao ya hali na mali, huku tukiwaombea marehemu wapumzike  kwa amani na majeruhi majeruhi wapate kupona haraka," amesema.

Kutokana na kiasi hicho kilichotolewa na Bank KCB pamoja na michango ambayo  wananchi na tasisisi mbalimbali zilizoguswa na kuchangia rambirambi katika maafa hayo imefikia jumla ya shilingi milioni 557
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive