Tume
 ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imesitisha masomo na udahili wa wanafunzi
 wapya kwa ngazi zote za masomo na katika programu kwenye baadhi ya vyuo
 vikuu kutokana na kukosa vigezo.
Pia imefuta vituo viwili vya vyuo vikuu na kuamuru wanafunzi wanaoendelea na masomo wahamishwe.
Akizungumza
 na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumanne Septemba 25, 
Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amevitaja vyuo hivyo 
kuwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala nchini (KIUT), 
Chuo cha Teofilo Kisanji (TEKU), Chuo Kikuu kishiriki cha Marian 
(MARUco) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Kardinali Rugambwa  
(CARUMUCo).
Vyuo
 vingine ni Chuo cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU), Chuo kikuu
 cha Mt. Yohana cha Tanzania (SJUT-St. Marks Centers na Chuo kikuu cha 
Umoja wa Afrika Tanzania (UAUT).
Vyuo
 hivyo ni pamoja na Chuo kikuu Teofilo Kisanji, Kituo cha Tabora  na 
Chuo kikuu Mt. Yohana cha Tanzania, Msalato (SJUT -Msalato Center).
Aidha,
 amevitaja vyuo vilivyositishiwa utoaji mafunzo na kuamuru wanafunzi 
wote wanaoendelea na masomo wahamishwe kuwa ni Mlima Meru (MMU), Chuo 
Kikuu cha Bagamoyo (UoB), Chuo cha Eckernforde Tanga (ETU) cha Kilimo na
 Teknolojia cha Jomo Kenyatta Kituo cha Arusha na Chuo Kikuu Kishiriki 
cha Josiah kibira (JOKUCo).
“Asitokee
 mwanafunzi yeyote akasajiliwa katika vyuo hivyo na wanaotakiwa kuhama 
wawasiliane na vyuo vyao haraka,” amesema Profesa Kihampa.
Kwa
 upande wake mwakilishi kutoka Bodi ya Mikopo (HELSB), Deus Changala 
amesema waliokuwa na mikopo wasiwe na wasiwasi itapelekwa watakapokuwa.






No comments:
Post a Comment