wanaotembeza chakula stendi ndogo kahama wapigwa stop


Halmashauri ya Mji wa Kahama imeshauriwa kuwadhibiti watu wanaotembeza chakula katika kituo kidogo cha mabasi Majengo ili kutoa fursa ya kupata wateja, kwa Mamalishe wanaouza chakula ndani ya jengo jipya la Mamalishe lililofunguliwa hivi karibuni katika kituo hicho.

Wakizungumza kwenye kipindi cha Raha ya Leo cha KAHAMA FM, Baadhi ya Mamalishe, wamesema ni vyema serikali ikawadhibiti watu hao ili kuongeza mapato ya ndani yanayotokana na mradi wa jengo hilo.

Mamalishe hao, VICTORIA MWETA, CHRISTINA KIDUBO, na DIANA VICENTY wamesema mbali na kudhibiti wauzaji hao, wameiomba halmashauri hiyo kuziondoa baadhi ya nyumba zilizopo mbele ya jengo hilo ili wateja waweze kuliona kwa urahisi.

Naye Mwenyekiti wa Mamalishe katika jengo hilo, RAHAMA JOHN amesema tayari wamewapa taarifa viongozi wa halmashauri ili kuboresha mradi huo huku akiwataka Mamalishe kuendelea kujituma katika kazi zao kwa lengo la kujiimarisha kiuchumi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mji wa Kahama ANDERSON MSUMBA amesema halmashauri hiyo itaendelea kuwapa mazingira bora na rafiki mama lishe wa eneo hilo ili kufanya biashara zao kwa ufanisi.

Jengo la mama lishe Majengo mjini Kahama limefunguliwa rasmi mwishoni mwa mwezi uliopita kwenye mbio za mwenge wa uhuru kitaifa likiwa na vyumba 12 vinavyotumiwa na mama lishe 24 na kwmaba limegharimu kiasi cha shilingi milioni 183.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive