Anthony Mavunde: Kilimo cha umwagiliaji kiwe kipaumbele kwa wakulima Halmashauri ya Mji Kahama


Halmashauri ya mji wa kahama mkoani Shinyanga imetakiwa kuwatengenezea miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji wakulima wake badala ya kuwapatia fedha katika vikundi ili kutengeneza kilimo chenye tija.

Ushauri huo umetolewa na Naibu waziri wa kazi, vijana, ajira na ulemavu ATHONY MAVUNDE alipokuwa akizungumza na wananchi wa kata ya mwendakulima, Katika Halmashauri hiyo wakati akikagua Mradi wa kilimo cha kisasa (GREEN HOUSE) Mradi ambao umetengwa kwa ajili kilimo cha mboga mboga.

Nao baadhi ya wakulima kutoka kata ya mwendakulima wamesema wanaukosefu wa mitaji, pembejeo, masoko, maeneo na ushirikishwajiki katika sekta mbalimbali za kiuchumi hali inayosabisha kushindwa kuendelea kumudu gharama za uendeshaji wa kilimo hicho.

Naye mkurugenzi mtendaji wa Halmashuri ya mji wa Kahama, ANDERSON MSUMBA amesema wanatoa mikopo kwa vijana na wanawake kwa kila kata kwa kufuata utaratibu na kanuni ili uweze kuwanufaisha walengwa wote.

Naibu waziri MAVUNDE amendelea na ziara ya siku moja katika Halmashauri ya Ushetu ikiwa na lengo la kukagua Mradi wa kilimo hicho cha kisasa cha (GREEN HOUSE)
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive