Jukwaa
 la Katiba Tanzania (Jukata) limelitaka Jeshi la Polisi na tume ya taifa
 ya Uchaguzi (NEC) kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na si kutumika 
kisiasa.
Kauli
 hiyo imetolewa jana Jumatano Septemba 19, 2018 na Mwenyekiti wa Jukata,
 Hebron Mwakagenda katika mkutano wake na waandishi wa habari ambapo 
amezungumzia hali ilivyokuwa katika uchaguzi wa Ubunge katika jimbo la 
Ukonga na Monduli pamoja na ule wa Udiwani katika kata 24.
Katika
 ufafanuzi wake Mwakagenda amesema amesikitishwa na kitendo cha baadhi 
ya polisi kushangilia uchaguzi kumalizika salama wakati waliotakiwa 
kufanya hivyo ni wananchi.
"Polisi
 wanashangilia hadharani bila aibu kuwa uchaguzi umefanyika kwa amani 
kwani nani alitakiwa kuhakikisha kwamba amani hiyo inakuwepo si wao, 
wanashangilia ushindi upi wakati ni wajibu wao kulinda mali raia na mali
 zao”, alisema Mwakagenda.
Akiwazungumzia
 NEC, Mwakagenda alisema tume hiyo haipaswi kupendelea upande wowote wa 
chama cha siasa ili kuepuka kasoro ambazo hujitokeza katika chaguzi 
mbalimbali ikiwemo za marudio, "Uchaguzi ni kama mechi, tume ndio refa 
kwa hiyo kama itapendelea upande mmoja mechi haiwezi kuwa ya amani”.
Uchaguzi
 huo umefanyika Septemba 16, 2018 ambapo baada ya matokeo kutangazwa , 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda na Polisi Kanda Maalum ya 
Dar es Salaam walipongezana hadharani kwa kulinda amani kabla na baada 
ya uchaguzi wa ubunge Jimbo la Ukonga, jambo ambalo katibu wa Itikadi na
 Uenezi CCM, Humphrey Polepole alilipinga.






No comments:
Post a Comment