Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga lakamata wawili kwa kujifanya Usalama wa Taifa

Image result for SIMON HAULE IMAGES



Jeshi la polisi Mkoa wa SHINYANGA linawashilikia watu wawili GOGADI SULEIMAN (62) na KILIMA MBWILIZA (49) kwa tuhuma ya kujifanya watumishi wa umma katika idara ya usalama wa taifa na kuwakuta na baadhi ya vitambulisho bandia vya usalama wa taifa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa SHINYANGA SIMON HAULE amesema watuhumiwa hao wamekamatwa majira ya saa 1:30 usiku mjini shinyanga na kukutwa na vitu feki mbalimbali ambavyo ni vya kiserikali.

Vitu walivyokutwa navyo watuhumiwa hao ni pamoja na fomu za maombi ya kazi idara ya usalama wa taifa, picha mbalimbali za watu, vipimo vya nguo (Suti), na Nyaraka mbalimbali za serikali

Kamanda HAULE amesema watuhumiwa hao wakati wanakamatwa walikutwa na binti mmoja ambaye walikuwa katika mazungumzo naye ya kumtaka awapatie Tsh. Mil 1 ili apewe kazi katika idara ya usalama wa taifa.

Jeshi la polisi Mkoa wa SHINYANGA linatoa wito kwa wanancho wote kuwa shughuli zote za serikali hufanyika katika ofisi za serikali zinazotambulika kisheria na sio katika maeneo mengine.

Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive