Mahakama 
 ya Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi, imemhukumu Ramadhani Shaban (24), 
Mkazi wa Mtaa wa Majengo B, kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kumtia 
hatiani kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 15, bubu ambaye 
pia ana upungufu wa akili.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Gosper Luoga, baada ya mshtakiwa kukiri kosa.
Awali,
 Mwendesha Mashtaka wa Serikali wa Mkoa wa Katavi, Flaviana Shio, alidai
 mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Septemba 9, mwaka huu
 majira ya saa 12 jioni katika Mtaa wa Majengo B.
Alidai
 kuwa siku ya tukio mshtakiwa alikwenda maeneo ya Mtaa wa Mjimwema 
alikokuwa akiishi mtoto huyo na mjomba wake, Ernest Chambala na kumpakia
 kwenye baiskeli yake.
Alisema alikwenda naye hadi kwenye chumba chake alichokuwa amepanga na kumbaka.
Aliendelea
 kuiambia mahakama kuwa baada ya tukio hilo mtoto huyo alitoka nje na 
kuanza kuwaonyesha watu kwa ishara kuwa amebakwa.
Mjomba
 wa mtoto huyo alianza jitihada za kumsaka mbakaji huyo kwa kumchukua 
mpwa wake huyo ambaye alimwongoza hadi kwenye nyumba alikofanyiwa unyama
 huo.
Alieleza
 kuwa majirani wa nyumba hiyo walipoulizwa kama walimuona mtoto huyo 
akiingizwa kwenye chumba cha mshtakiwa walikiri kumuona.
Baada
 ya kukamatwa alichukuliwa na kupelekwa kituo cha polisi na katika 
maelezo yake alikiri kutenda kosa hilo na taarifa za daktari 
zilithibitisha kuwa mtoto huyo alikuwa ameingiliwa na mwanaume kwa kuwa 
sehemu zake za siri zilikuwa na mbegu za kiume.
Mshtakiwa alikiri kutenda kosa hilo kwa kile alichodai amekuwa akifanya naye mapenzi mara kwa mara kwa sababu ni mpenzi wake.
Katika
 utetezi wake, mshtakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa 
mama yake mzazi anamtegemea na baba yake alishafariki.
Hakimu
 Luoga baada ya kusikiliza utetezi huo aliiambia mahakama kuwa mshtakiwa
 amepatikana na hatia imemhukumu kwenda kutumikia jela miaka 30.
Alisema katika hukumu hiyo mahakama pia imezingatia ongezeko la matukio ya ubakaji wilayani humo.






No comments:
Post a Comment