Waziri 
 wa Nchi, Ofi si ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 
(Tamisemi), Selemani Jafo amewaagiza maofi sa wa elimu wa mikoa na 
wilaya kuzingatia maadili kwa kuepuka vitendo vya upendeleo na 
unyanyasaji wa walimu na wanafunzi.
Pia
 amewataka kujiepusha na suala la uvujishaji mitihani, rushwa na utovu 
wa maadili. Katika hotuba yake iliyosomwa na Naibu Waziri Joseph Kakunda
 wakati wa kufungua kikao kazi cha siku mbili kilichowakutanisha maofisa
 elimu wa mikoa na halmashauri kilichofanyika jijini hapa, Jafo 
alihimiza umuhimu wa kuzingatia maadili na kusisitiza kuwa siku za hivi 
karibuni, sekta hiyo imejijengea picha mbaya kwa mambo kadhaa.
“Tunatakiwa
 kuepuka vitendo vya upendeleo na unyanyasaji wa aina yoyote kwa walimu 
na wanafunzi, uvujaji wa mitihani, rushwa na utovu wa maadili kwa sababu
 ninyi ni kioo cha jamii,” alisema. 
Jafo
 alionya kuwa vitendo vya utovu wa maadili kamwe havitavumiliwa na 
serikali na yeyote anayeendekeza vitendo hivyo atachukuliwa hatua kali.
“Nitumie fursa hii kulaani vitendo vya unyanyasaji na ukatili vilivyofanywa na baadhi walimu katika Shule ya Msingi Kibeta.”
 Aidha, Jafo aliwaasa viongozi hao kusimamia sheria, kanuni na taratibu katika utoaji wa adhabu kwa wanafunzi kote nchini. 
Alitumia
 nafasi hiyo kutoa msisitizo kwa viongozi hao kuwajibika kwa kufanya 
kazi kwa bidii, weledi na kuitumikia umma, watumishi, wadau na marafiki 
wa elimu ili kuendeleza imani iliyojengwa kwa umma.
Mkutano
 huo umewakutanisha watendaji wa elimu katika ngazi ya taifa, mikoa na 
halmashauri kwa lengo la kukumbushana majukumu, kujipima na kujitafakari
 utendaji, kupeana uzoefu, kujenga uwezo na kujadiliana juu ya mbinu na 
mikakati itakayotumika kusaidia kuboresha utoaji wa elimu bora.






No comments:
Post a Comment