
Waziri 
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka viongozi na watumishi
 mbalimbali wa wizara yake wafanye kazi kwa kushirikiana na kuacha tabia
 ya kunyanyasana wakati wanatekeleza majukumu yao ya kikazi.
Lugola
 pia amesema kila mtumishi wa wizara yake ana umuhimu mkubwa kwa 
kufanikisha mafanikio ya wizara hiyo kwakuwa watumishi hao wanafanya 
kazi kwa kutegemeana. 
Akizungumza
 na watumishi wa makao makuu wa wizara hiyo katika ukumbi wa mikutano wa
 Chuo cha Veta, jijini Dodoma jana, Lugola alisema kikao hicho 
alikiitisha kwa lengo la kujuana na watumishi hao pamoja na kujua 
changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi.
“Mambo
 muhimu ambayo yatatuletea mafanikio ndani ya wizara yetu ni kufanya 
kazi kwa bidii, kufanya kazi kwa kushirikiana na tukifanya hivyo hakika 
tutapendana na kuzidi kufanikiwa,” alisema Lugola.
Lugola
 aliongeza kuwa, hapendi kuona mtumishi yeyote ananyanyaswa kwa kutopewa
 haki zake au kucheleweshewa pasipo kuwa na sababu za msingi ikiwemo 
malipo mbalimbali ya watumishi wanayodai, na endapo yatatokea hayo 
watumishi hao wamletee kero zinazowakabili ofisini kwake na kwa 
kushirikiana na katibu mkuu wa wizara hiyo watazitatua.
“Utumishi
 wa umma naujua, na pia nimepitia manyanyaso kadhaa mpaka leo nimefikia 
hapa kutokana na historia yangu, kwanini tusipendane?, kwanini 
tunyanyasane?, kwanini tusishirikiane?, ni tabia mbaya na inatakiwa 
kulaaniwa kwa baadhi ya wakuu wa idara na vitengo pamoja na wengineo 
ambao wanatabia ya kunyanyasa watumishi waliochini yao,” alisema Lugola.
Mkutano
 huo ambao ni wa kwanza kwa Waziri Lugola, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo 
Meja Jenerali, Jacob Kingu pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan 
Kailima, kuzungumza na watumishi wa Wizara hiyo tangu walipoteuliwa 
miezi kadhaa iliyopita, walitaka kujuana zaidi na watumishi wa wizara 
hiyo pamoja na kujua changamoto zao zinazowakabili. Toggle screen reader
 support 
Credit: 
Felix Mwagara
Felix Mwagara






No comments:
Post a Comment