Zoezi 
 la ukoaji wa miili ya watu waliopoteza maisha katika Kivuko cha MV 
Nyerere limeanza rasmi baada ya kusimama jana usiku, ambapo Vikosi 
Maalum vya uokoaji vya Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa 
Watanzania (JWTZ) na Jeshi la Zimamoto na uokoaji vinaendesha zoezi 
hilo.
Hadi
 sasa idadi ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo 
iliyotokea jana tarehe 20 Septemba 2018 imeongezeka kutoka watu 44 hadi 
86.
Kivuko cha MV Nyerere kilizama katika Ziwa Victori kikitokea Bugorora kisiwani Ukerewe kuelekea Kisiwa cha Ukara.
Inahofiwa
 kuwa, mamia ya watu waliokuwamo katika kivuko hicho wamepoteza maisha, 
ambapo watu 37 walifanikiwa kuokolewa wakiwa hai hapo jana.
Mkuu
 wa Wilaya ya Ukerewe Cornel Maghembe amesema kuwa sababu ya kuzama kwa 
kivuko hicho inasadikika kuwa ilibeba watu zaidi ya 400 ambapo 
kilizidisha uwezo wake ambao ni watu 101.
Maghembe amesema kuwa imezama mita chache kabla ya kuwasili eneo la Ukara ambapo dereva alipunguza mwendo kuashiria amekaribia kutia nanga ndipo abiria wengi walihamia upande wa lango la kutokea wakiwahi kusogea ili washuke ndipo uzito ulizidi na kupinduka.
“Abiria walipoona mwendo umepunguzwa walikimbilia kuwahi mbele ya lango ili kujiandaa kushuka, ndipo uzito ukaegemea upande mmoja”, amesema Maghembe
Maghembe amesema kuwa imezama mita chache kabla ya kuwasili eneo la Ukara ambapo dereva alipunguza mwendo kuashiria amekaribia kutia nanga ndipo abiria wengi walihamia upande wa lango la kutokea wakiwahi kusogea ili washuke ndipo uzito ulizidi na kupinduka.
“Abiria walipoona mwendo umepunguzwa walikimbilia kuwahi mbele ya lango ili kujiandaa kushuka, ndipo uzito ukaegemea upande mmoja”, amesema Maghembe






No comments:
Post a Comment