Imeelezwa
 kuwa sehemu pekee ya kuimarisha kilimo cha mwananchi mmoja mmoja, 
wananchi katika makundi ya kijamii hususani vijana ni kupitia sekta ya 
kilimo kwani ndio sehemu pekee ya ukombozi wa mkulima katika jamii.
Imeelezwa
 kuwa kuna uwezekano wa kufanya biashara mbalimbali nchini ambazo 
zinaweza kuongeza kipato lakini sahemu sahihi isiyokuwa na jazba na 
dhoruba katika utendaji ni kufanya kilimo biashara ambacho kamwe 
hakiwezi kumtupa mkulima.
Dkt
 Charles Tizeba Waziri wa kilimo, ameyasema hayo leo tarehe 25 Septemba 
2018 wakati akizungumza na vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha 
Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga ambao wapo katika kambi maalumu ya 
ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Vijana
 hao ambao wameamua kutumia nguvu zao pasina malipo wameamua kwa umoja 
wao kuunga mkono juhudi za Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa 
kauli yake inayohamasisha chachu na juhudi za kiutendaji kwa wananchi ya
 “Hapa Kazi Tu”.
Aidha,
 katika kuhamasisha juhudi za kiutendaji Waziri huyo mwenye dhamana ya 
kilimo ameunga mkono juhudi za vijana hao kwa kuchangia fedha ya chakula
 shilingi 1,100,000 sambamba na kushiriki ujenzi wa jengo maalumu la 
upasuaji.
Waziri
 wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba alitembelea ujenzi huo wa Hospitali ya
 Wilaya ya Muheza akiwa safarini kutembelea mashamba ya mkonge ikiwa ni 
siku ya pili ya ziara ya kikazi Mkoani Tanga aliyoianza jana tarehe 25 
Septemba 2018 ya kukutana na makundi mbalimbali ya wakulima wa zao la 
Mkonge ili kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili wakulima wa 
zao hilo.






No comments:
Post a Comment