Wakazi Mtaa wa Majengo Kahama waiomba serikali kuimarisha mitaro ya maji kukinga nyumba zao kuharibiwa

Related image

Baadhi ya Wananchi wa Mtaa wa Majengo katika Halmashauri ya Mji wa Kahama wameiomba halmashauri hiyo kujenga na kuiimarisha mitaro ya maji katika barabara zote za mitaa ili kuzuia maji ya mvua yasielekee kwenye makazi ya watu.

Wakizungumza leo kwenye kipindi cha Raha ya leo, kinachorushwa na Kahama Fm baadhi Wananchi hao wamesema bado barabara nyingi za mitaa hazipitiki kutokana na kuharibiwa na mvua wakati wa masika na kwamba hali hiyo pia inahatarisha afya zao.

Katika hatua nyingine wananchi hao wameishauri serikali kuiangalia kwa jicho la pili kata ya Majengo katika suala la utiririshaji wa maji machafu yanatoa harufu mbaya na kuhatarisha afya za wananchi wa mtaa huo.

Diwani wa Kata ya Majengo BERNAD MAHONGO amesema ujenzi wa mitaro katika kata ya Majengo unaendelea kufanyika katika maeneo yote korofi ili kuzuia maji yasituame na kusambaa kwenye makazi ya watu.

Kata ya Majengo ni miongoni mwa Kata za halmashauri ya Mji wa Kahama ambazo zimekuwa zikikumbwa na athari ya maji ya mvua kuingia kwenye makazi ya watu jambo ambalo limekuwa likileta hofu na kuhatarisha usalama na afya za wananchi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive