Benki Kuu ya Tanzania imewataka wananchi kuheshimu fedha ya Tanzania kwani ni moja ya alama ya taifa.
Kauli
 hiyo imekuja kufuatia matukio ya hivi karibuni ya baadhi ya wananchi 
kutoziheshimu, kuzifanyia dhihaka na kebehi noti za Jamhuri ya Mungano 
wa Tanzania.
Taarifa
 ya BoT kwa vyombo vya habarI ambayo inasema utunzaji mzuri wa fedha 
zetu utapunguza uwezekano wa fedha hizo kuchakaa mapema na kupunguza 
gharama za uchapishaji.
"Kwa
 mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006, kifungu cha 
26, BoT ndiyo taasisi pekee yenye mamlaka ya kutoa noti na sarafu katika
 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," imesema taarifa hiyo.
Pia
 imesema noti na sarafu hizo zina alama muhimu inayolitambulisha taifa 
la Tanzania ambayo ni nembo ya Bwana na Bibi. Imefafanua alama hiyo 
inapaswa kuheshimwa kama zilivyo alama nyingine kwa mfano Bendera ya 
Taifa.
Pia
 noti na sarafu zote zimetengenezwa kutoa thamani ya kisheria (legal 
tender) kama ilivyoandikwa juu ya noti au sarafu husika na pia Benki Kuu
 pekee ndiyo yenye mamlaka ya kuharibu noti na sarafu.
Taarifa
 hiyo imefafanua kuhusu hilo kupitia kifungu cha  28 kikisomwa pamoja na
 kifungu cha 30 cha Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006.
"Benki Kuu inatoa rai kwa wananchi kuzitunza fedha zetu kwa kuwa ni mojawapo ya tunu na alama muhimu ya uchumi wa nchi yetu.
"Benki Kuu inatoa rai kwa wananchi kuzitunza fedha zetu kwa kuwa ni mojawapo ya tunu na alama muhimu ya uchumi wa nchi yetu.






No comments:
Post a Comment