Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi amewataka watumishi wa wizara hiyo kufanyakazi kwa weledi ili kuogeza tija kwa Taifa.
Katibu
 mkuu huyo ametoa rai hiyo leo, Septemba 25, 2018 alipokuwa akiwaaga 
watumishi wa wizara baada ya kustaafu jeshini na kwa mujibu wa sheria 
tangu Septemba 16.
Milanzi
 amesema kwa muda wote aliitumikia wizara hiyo alipata ushirikiano wa 
kutosha uliomuwezesha kuiongoza vyema wizara hiyo na kuchangia mafanikio
 yaliyojidhihirisha kwenye sekta za wanyamapori, utalii, misitu na nyuki
 na malikale.
Katika kipindi cha uongozi wake wizarani hapo, amesema wizara imepata mafanikio katika  vita dhidi ya ujangili.
“Tumekamilisha
 mambo mengi. Kila mmoja wenu alikuwa akinisaidia ili wizara isonge 
mbele. Hakuna aliyetaka kunikwamisha. Ninawashukuru sana,” amesema 
Milanzi.
Akizungumza
 kwenye hafla fupi ya kumuaga Milanzi iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa
 Chuo Kikuu cha Dodoma, kaimu katibu mkuu wa wizara hiyo, Dk Aloyce 
Nzuki amempongeza kwa utumishi wake.
“Umeweka
 mifumo mizuri na kubuni mikakati na mbinu za kutatua changamoto 
zilizokuwa zinaikabili wizara na kuhakikisha watumishi wanapata utulivu 
wa akili kwa kujali maslahi yao. Uliwawezesha kufanya kazi wakiwa 
watulivu wa akili jambo liliongeza ufanisi kazini,” ameeleza Dk Nzuki.
Milanzi aliteuliwa kuwa katibu mkuu wa wizara hiyo Disemba 2015. 
“Nashukuru
 nimestaafu salama. Wizara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi na 
inagusa masilahi ya wengi. Jukumu nililopewa lilikuwa kusimamia maslahi 
ya nchi, naamini kuna masilahi ya watu yalivurugwa hivyo mimi kuwa mwiba
 kwao,” amesema akiaga kamanda huyo wa Jeshi la Wananchi (JWTZ).






No comments:
Post a Comment