
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe 
amebainisha kuwa lugha ya Kiswahili inatarajiwa kuwa lugha kuu ya 
mawasiliano katika bara la Afrika ifikapo mwaka 2063.
Waziri
 Mwakyembe ameyasema hayo jana Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza 
na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Kampeni Ya Uzalendo na 
Utaifa kwa mwaka 2018 yanayotarajiwa kufanyika Desemba 8 Jijini Dodoma 
ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais John Pombe Magufuli.
Alisema
 kuwa kampeni hiyo kwa mwaka huu imejikita katika kuhamasisha matumizi 
ya lugha ya Kiswahili ambayo ni kielelezo kikubwa cha utashi na uhai wa 
taifa la Tanzania na inakua kwa kasi sana barani Afrika na duniani kote 
kwa ujumla.
“Sasa
 hivi Kiswahili ni lugha ya kumi kati ya lugha elfu 6 zinazoongelewa na 
watu wengi duniani na kwa mujibu wa Tafiti za Umoja wa Afrika zinaonesha
 kuwa ifikapo mwaka 2063 Kiswahili kitakuwa lugha kuu ya mawasiliano 
katika bara la Afrika na utambulisho wa mtu mweusi duniani,” alisema 
Mwakyembe.
Alieleza
 kuwa dunia yote inatambua kwamba Tanzania ndio chimbuko la lugha adhimu
 ya Kiswahili hivyo watanzania wanapaswa kujivunia lugha hiyo na 
kuitangaza kwa kuwa ni sehemu ya utamaduni wa taifa na msingi wa 
uzalendo na utaifa.
Waziri
 Mwakyembe alibainisha kuwa kampeni hiyo mwaka huu imejikita katika 
kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili ili kuwasisitiza watanzania 
kuthamini lugha yao na utamaduni wao na kurejea kwenye misingi ya 
maadili ya taifa lao.
Alisema
 kuwa sasahivi kuna changamoto kubwa ya mmomonyoko wa maadili 
inayosababishwa na baadhi ya watu hasa vijana kuiga tamaduni za nje 
kutokana na utandawazi hivyo kupelekea kudharau utamaduni wao ikiwemo 
lugha ya Kiswahili jambo ambalo lisipochukuliwa hatua madhubuti litaleta
 athari kwa jamii.
Pia
 Waziri Mwakyembe alitoa pongezi kwa Rais John Pombe Magufuli kwa 
mchango wake mkubwa anaoonesha katika kutumia, kukuza na kuitangaza 
lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi hivyo amekuwa ni mfano wa 
kuigwa.
Aidha
 alitoa rai kwa watanzania wote na wadau mbalimbali kuunga mkono kampeni
 hiyo kwa hali na mali ili Tanzania iweze kufanikiwa kulinda misingi ya 
utamaduni na utaifa hususan lugha ya Kiswahili.
Kampeni
 ya Uzalendo na Utaifa ilianza rasmi mwaka jana 2017 na itakuwa 
ikiadhimishwa kila mwaka ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu yake ni 
‘Kiswahili Uhai Wetu, Utashi Wetu’.  






No comments:
Post a Comment