HALMASHAURI YA MSALALA - KAHAMA YATENGA MIL. 15 ZA PIKIPIKI ZA MAAFISA UGANI KURAHISISHA UTENDAJI

Image result for pikipiki mpya
Na Salvatory Ntandu
KAHAMA

Halmashauri ya MSALALA Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA imetenga shilingi milioni 40 ili kununua pikipiki 15 za Maafisa Ugani ili kurahisisha utendaji kazi.

Kauli hiyo imetolewa jana Afisa kilimo wa Halmashauri ya Msalala ZEDEKIA SOLOMONI wakati akiwasisha Mada kwenye Warsha ya siku mbili iliyoandaliwa Shirika lisilo la kiserikali la CABUIPA kwa kushirikiana na shirika la OXFAM iliyofanyika Mjini Kahama.

Amesema katika mwaka wa fedha wa 2018/19 Wametenga fedha hizo ili kutekeleza agizo la Serikali la kuwapatia Maafisa ugani Usafiri ili kutoa huduma bora za kilimo kwa wakulima katika maeneo yao.

Katika Hatua nyingine ZEDEKIA amewataka Wakulima kuzingatia Maelekezo ya Serikali juu ya Mabadiliko ya Tabia nchi kwa kupanda Mazao yanayostahimili ukame na kuachana na kilimo cha Mazoea.
Mradi wa kupunguza athari za maafa na majanga unatekelezwa na shirika la CABUIPA kwa kushirikiana na Shirika la Misaada la Uingereza (OXFAM) katika Halmashauri hiyo kwa miaka miwili kwa lengo la kupunguza ukame kwa kuwapatia wananchi elimu juu ya mabadiliko ya tabia nchi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive