AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA WIZI

Image result for MAHAKAMANI NYUNDO
Na Lilian Katabaro
KAHAMA.

Mkazi wa mtaa wa Nyasubi Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga DENICE KIZENGA (21) amefikishwa mbele ya Mahakama ya Wilaya hiyo kwa tuhuma ya wizi wa kuaminika kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo USHINDI SWALO mwendesha mashitaka wa Polisi SAADA ADAM amesema KIZENGA alitenda kosa hili Septemba 4 mwaka huu majira ya saa 2 asubuhi huko mtaa wa majengo aliiba belo mbili za vitenge zenye thamani ya shilingi 3,800,000 mali ya DAUD RICHARD.

SAADA amesma KIZENGA ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 273 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Katika shauri hilo la jinai namba 32/2018 KIZENGA amekana kutenda kosa hilo na upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na mshitakiwa amerudishwa rumande kwa kukosa dhamana na shauri hilo kutajwa tena Mahakamani hapo Septemba 25 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive