WAWILI WAFIKISHWA MAHAKANI KWA TUHUMA ZA KUJIPATIA FEDHA KWA NJIA YA UDANGANYIFU


Na Lilian/Paulina
KAHAMA.
 
Wakazi wawili wa wilayani KAHAMA, JUMA MASALAGO (27) na RODA EMMANUEL (29) jana Wamefikishwa katika mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma ya kujipatia shilingi laki moja kwa njia ya udanganyifu.

Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, EVODIA KYARUZI Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU Kahama KELVIN MURUSURI amesema watuhumiwa hao walikamatwa Mwezi March mwaka huu wilayani Kahama.

MURUSURI amesema MASALAGO na EMMANUEL walitenda kosa hilo mwezi machi mwaka huu ambapo walijipatia shilingi laki 3 ili waweze kumsaidia JOHN MABARA katika kesi yake namba 153/2017 ambayo ipo katika baraza la Ardhi na nyumba wilayani Kahama ili ashinde.

Aidha MASALAGO anashitakiwa kwa kosa jingine kujifanya mtumishi wa serikali katika baraza la Ardhi hivyo March 27 mwaka huu alipatia sehemu ya pesa hizo kiasi cha shilingi laki 104,000/=

Katika shauri hilo la jinai namba 179/2018 MASALAGO amefanya kosa kinyume na kifungu 100 b cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2012.

Aidha EMMANUEL anakabiliwa na shitaka la rushwa kinyume na kifungu 15 na 2 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

MASALAGO amekana kutenda makosa hayo huku EMMANUEL akikiri simu yake kupokea kiasi hicho cha pesa na Shauri hilo limeahirishwa hadi May 29 mwaka huu litakapotajwa tena kwa ajili ya usikilizwaji wa awali na wamerudishwa rumade kwa kukosa dhamana.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive