WATENDAJI 35 WA MITAA NA KATA AMBAO WALIKUWA WAMESITISHIWA AJIRA ZAO KUTOKANA NA KUWA NA ELIMU YA DARASA LA SABA WAREJESHWA KAZINI


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Halmashauri ya Mji wa KAHAMA Mkoani SHINYANGA jana imewarejesha kazini maafisa watendaji 35 wa Mitaa na Kata ambao walikuwa wamesitishiwa ajira zao kutokana na kuwa na elimu ya darasa la Saba.

Akizungumza na KAHAMA FM Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, ANDERSON MSUMBA amesema zoezi hilo ni utekelezaji wa agizo la serikali.

Kuhusu malipo ya mishahara yao ambayo walikuwa hawajalipwa tangu watolewe kwenye mfumo wa ajira, MSUMBA amesema kwanza wanawaingiza kwenye mfumo rasmi ili zoezi la kuwalipa liendelee na kwamba kila Mtendaji ataendelea na cheo alichokuwa nacho awali.

Mmoja wa Maafisa watendaji hao, SIMON MABUMBA akizungumza kwa niaba ya wenzake, ameishukuru serikali kwa kuwarudisha kazini ambapo ameahidi watafanyaka kazi ya umma kwa bidii ikiwamo kusimamia kikamilifu miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao ya kazi.

Hivi karibuni serikali iliagiza kurejeshwa kazini maafisa wote watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata waliokuwa wameajiriwa kabla ya mei 20 , 2004, ambao walikuwa wameondolewa kwenye ajira kutokana na kukosa sifa ya kuwa na elimu ya kidato cha nne.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive