WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA WALIOKOPA WILAYANI KAHAMA WATAKIWA KUUZA PAMBA ZAO KATIKA VYAMA VYA MSINGI ILI KUINGIZWA KWENYE KUMBUKUMBU NA KUJENGA UAMINIFU KATIKA MSIMU UJAO


Na Amina Mbwambo
KAHAMA.

Wito umetolewa kwa wakulima wa zao la pamba waliokopa Wilayani KAHAMA kuhakikisha wanauza pamba zao katika vyama vya msingi na makampuni waliyokopa ili kuingizwa kwenye kumbukumbu na kujenga uaminifu katika msimu ujao.

Akizungumza na kahama fm leo, mwenyekiti wa chama cha ushirika cha Kahama (KACU) ambaye anasimamia zao la pamba na tumbaku, EMANUEL CHARAHANI amesema msimu wa zao la pamba utafunguliwa rasmi kesho na hivyo na kuwataka wakulima.

CHARAHANI amesema pamoja na kufunguliwa kwa msimu huo serikali imeelekeza malipo yote ya pamba kufanyika kwa njia ya benki na hivyo kila mkulima kwa kushirikiana na maafisa ushirika wa maeneo husika ahakikishe anafungua account kwa ajili ya malipo na usalama wa fedha zao.

Akizungumzia mfumo huo mpya wa ununuzi wa pamba, mkuu wa wilaya ya Kahama, FADHILI NKURLU amesema maandalizi yote ya ununuzi wa pamba yamekamilika na amewataka wakurugenzi na maafisa ushirika kuyatambua maeneo yote yatakayotumika katika ununuzi wa pamba na kuyatangaza.

Msimu wa zao la pamba unafunguliwa rasmi kesho Mei mosi ambapo kitaifa utafunguliwa katika wilaya ya Igunga mkoani Tabora ambapo serikali imeiagiza mikoa yote inayolima pamba nchini kuhakikisha ununuzi wa pamba yote unafanyika kwa njia ya account.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive