VYOO CHANGAMOTO MACHIMBO YA DHAHABU YA KALYANGO KAHAMA



Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Idara ya Afya na usafi wa Mazingira katika machimbo ya dhahabu ya Kabela Ilindi, Kata ya Zongomela Wilayani KAHAMA imeiagiza kampuni ya Kalyango Gold Mine kujenga vyoo vingi zaidi ili kuzuia mlipuko wa magonjwa unaoweza kujitokeza.

Akizungumza na KAHAMA FM, Mkuu wa idara ya afya na usafi wa mazingira katika katika machimbo hayo, MACHIMU NELSON amesema idara yake imajizatiti kuhakikisha kila machimbo yanakuwa na vyoo vya kutosha.

Naye Meneja wa Kampuni ya Kalyango Gold Mines, MDAKI SHABAN amesema tayari wameanza kujenga matundu mawili ya vyoo na bafu na kwamba wanaendelea kutenga fedha zaidi kwa ajili ya kuongeza matundu mengine ya vyoo.

Naye Msimamizi wa idara ya Afya na usafi wa mazingira katika machimbo hayo ya dhahabu ya Kabela Ilindi, DANI MUSSA amesema wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi waishio kwenye machimbo ili kuimarisha usafi wa mazingira katika machimbo hayo kwa manufaa ya jamii nzima.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive