ELIMU YA UZAZI KWA WANAFUNZI MKOANI SHINYANGA YAWA KIKWAZO



Na salvatory ntandu
KAHAMA.

Kukosekana kwa elimu ya Afya ya uzazi na uelewa kuhusu Balehe kwa wanafunzi katika shule za msingi na Sekondari Mkoani SHINYANGA kunasababisha wengi wao kujiingiza katika vishawishi na uasherati wakiwa katika umri mdogo.

Hayo yamebainishwa kwenye kongamano lililojumuisha wanafunzi 120 kutoka shule nane zilizopo katika kata Usanda halmashauri ya wilaya ya Shinyanga (Vijijini) ili kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya afya ya uzazi na jinsia yaliotolewa na shirika lisilo la kiserikali la AGAPE.

Akizungumza na wanafunzi hao Afisa wa Mradi wa Elimu ya Afya ya Uzazi na Ujinsia kwa Vijana kutoka AGAPE LUCY MAGANGA amesema elimu hiyo ikitolewa shuleni itawasaidia kujiepusha na tabia hatarishi zinazoweza kusababisha wakapata mimba na magonjwa ya zinaa ukiwemo Ukimwi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji AGAPE, JOHN MYOLA amesema vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinasababisha ndoto za watoto kutotimia hivyo kuitaka jamii kuungana katika kuhakikisha haki za watoto zinalindwa.

Katika hatua nyingine amewataka wazazi na walezi kutengeneza urafiki na watoto ili kujua matatizo wanayokutana nayo ikiwemo kufanyiwa ukatili na watu wa karibu waliopo katika jamii inayowazunguka.

Naye Afisa Elimu kata ya Usanda ESSERO ASHERY amesema ataendelea kuhamasisha walimu na viongozi mbalimbali kutoa elimu juu ya masuala ya afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana.

Nao baadhi ya wanafunzi waliohudhuria Kongamano hilo MUSA RAJAB na JENIFA SHIJA wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi katika shule mbalimbali ili kuwawezesha kutimiza malengo yao katika elimu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive