MADIWANI WA HALMASHAURI YA MSALALA WAAZIMIA KUVUNJA MKATABA NA KAMPUNI YA BAHARI PHARMACY NDANI YA SIKU 14


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama limeazimia kuvunja mkataba na kampuni ya BAHARI PHAMACY ndani ya siku 14 kuanzia leo baada ya kampuni hiyo kushindwa kutekeleza zabuni ya kusambaza dawa kwenye zahanati na vituo vya afya katika halmashauri hiyo.

Akitangaza hatua hiyo katika kikao cha baraza la Madiwani leo, mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, SIMON BEREGE amesema watazingatia sheria za kuvunja mkataba na mzabuni huyo na kwamba zabuni zijazo zitatolewa kwa muda wa majaribio ili kupima uwezo na utendaji kazi wa mzabuni.

Akizungumza katika kikao hicho, Diwani wa kata ya Isaka, GERALD MWANZIA amesema Mzabuni huyo ameshindwa kuzingatia mkataba unavyoelekeza huku diwani wa kata ya Busangia, ALEXANDER MIHAYO akiitaka serikali kuchukua hatua stahiki.

Naye katibu tawala msaidizi, serikali za mitaa, Mkoa wa Shinyanga, ALPHONCE KASANYI amesema atayafikisha maazimio ya baraza hilo la Madiwani la Halmashauri ya Msalala kwenye ngazi ya mkoa kwaajili ya utekelezaji.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive