WAKAZI WA NYAHANGA WILAYANI KAHAMA WAISHAURI SERIKALI KUIMARISHA MITARO INAYOPITISHA MAJI MACHAFU KUWANUSURU NA MAGONJWA YA MLIPUKO


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Baadhi ya wananchi wa vitongoji vya Maliasili A na B, Kata ya NYAHANGA Halmashauri ya Mji wa KAHAMA wameishauri serikali kuimarisha mitaro ya barabara katika vitongoji hivyo, ili kudhibiti maji ya mvua yasiingie kwenye makazi yao.

Wakizungumza kwenye kipindi cha Raha ya leo, baadhi ya wananchi hao wamesema ili kuzuia maji yasiende kwenye makazi yao ni lazima kujenga mitaro imara kwenye barabara hizo ili kuyaelekeza maji ya mvua yapite bila kuathiri makazi yao.

Wakati huo huo, Wananchi wa kitongoji cha Mlimani Mtaa wa Bukondamoyo mjini Kahama leo wameanza kumwaga vifusi vya changarawe kwenye barabara waliyojitolea kutengeneza ili kuunganisha na barabara kuu ya kwenda Mjini Kahama.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Bukondamoyo, JOSHUA YOHANA amesema wanategemea kumwaga tripu saba za changarawe ambazo zimetolewa kwa nguvu za wananchi wa Kitongoji hicho na wadau wengine.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive