ZOEZI LA UPIGAJI CHAPA KWA NG'OMBE LAINGIA DOSARI HALMASHAURI YA USHETU


Na Samwel Nyahongo
KAHAMA.

Zoezi la upigaji chapa kwa ng’ombe katika Halmashauri ya USHETU limekuwa tatizo kutokana na chapa zinazotumika kufanyia zoezi hilo kutokua katika ubora na usahihi unaofaa kitendo kinachosababisha ngombe hao kuungua au alama ya chapa hizo kuwahi kufutika.

Akitoa hoja hiyo katika Baraza la Madiwani la robo ya tatu la Halmashauri hiyo Diwani wa kata ya Ukune DAUDI MKOPA amesema upigaji chapa kwa mifugo hiyo imekua ni changamoto kwani chapa hizo hazipo kwenye ubora unaofaa.

MKOPA amesema maboresho ya chapa hizo unahitajika ili kuhakikisha wafugaji hawakwepi zoezi hilo kwa sababu kwamba chapa katika mifugo yao zinafutika, kitendo kitakachofanya wakwepe kulipa kodi kwa ajili ya kuchapa mifugo yao.

Akijibu hoja hiyo Katibu wa Baraza hilo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo MICHAEL MATOMORA amekiri kuwepo na changamoto hiyo kutokana na namba za chapa hizo kukaribiana kitendo kinachofanya ng’ombe kuungua.

MATOMORA amesema wao kama Halmashauri wameshatoa taarifa wilayani kuomba marekebisho ya chapa hizo ili kuzuia mifugo kuungua.

Katika hatua nyingine MATOMORA amesema kwa wafugaji ambao walipiga chapa na zikafutika, kumbukumbu zipo hivyo wakati wa marudio ya upigaji wa chapa hizo hawatarudia kulipa kodi ya upigaji chapa mara mbili.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive