VIONGOZI WA KATA KAHAMA WAAGIZWA KUUNDA VIKUNDI VYA ULINZI SHIRIKISHI KUDHIBITI VIBAKA


Na Amina Mbwambo
KAHAMA.

Serikali Wilayani KAHAMA imewaagiza viongozi wa kata na vijiji kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo yao kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi ili kulisaidia jeshi la polisi kupambana na wimbi la vibaka lililoibuka wilayani humo.

Akizungumza na KAHAMA Fm Mkuu wa Wilaya ya KAHAMA na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi Wilayani, humo FADHILI NKURLU amewataka wananchi kutokuwa na hofu na watoe taarifa za uhalifu ili kurahisisha operesheni inayoendelea dhidi ya vibaka wilayani humo.

Hivi karibuni, kumeibuka wimbi la vibaka mjini Kahama ambao wamekuwa wakiiba vitu mbalimbali zikiwemo betri za gari, kupora simu za mikononi pamoja na kuvunja nyumba na kuiba samani za ndani hali inayowafanya wananchi kuishi kwa mashaka.

WAKATI HUO HUO serikali wilayani Kahama imetoa onyo kali kwa wamiliki wa bar na vilabu vya pombe wilayani humo ambao wanakiuka taratibu za muda wa kufungua na kufunga sehemu hizo za starehe kulingana na vibali vyao.

Akiwaapisha Wakuu wapya wa mikoa Machi 16, 2016 Ikulu Dar es Salaam, Rais MAGUFULI aliwaagiza kuhakikisha baa zinafunguliwa saa 10 jioni na kufungwa saa 5 usiku, sambamba na kudhibiti mchezo wa pool table kwa kuwa unawadumaza vijana na kushindwa kufanya kazi.
Share:

1 comment:

  1. WAKAMATWE KWA HARAKA ZAIDI ILI KUPELEKWA MAHAKAMANI

    ReplyDelete

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive