VYAMA VYA USHIRIKA VILIVOKUFA KATIKA HALMASHAURI YA USHETU VYATAKIWA KUFUFULIWA


Na Samwel Nyahongo
KAHAMA.
 
Vyama vya ushirika vya pamba katika Halmashauri ya USHETU Wilayani KAHAMA vimetakiwa kufufua vyama vyao vilivyokufa katika kata mbalimbali ndani ya halmashauri hiyo kwa lengo la kuwarahisishia wakulima kwani msimu wa pamba umekwisha funguliwa.

Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo Diwani wa kata ya Nyankende DOWA LIMBU amewaomba viongozi wa chama cha ushirika kutafuta njia ya kuwasaidia wakulima wa pamba kwani msimu wa mavuno ya pamba unaendelea.

DOWA amesema njia nzuri ya kuwasaidia wakulima hao ni kuanzisha vituo kwa kila kijiji ili kuwapa wepesi wakulima pamoja kijiji husika kukusanya ushuru wa mapato kutokana na zao hilo.

Akijibu hoja hiyo Afisa Ushirika wa Pamba katika halmashauri hiyo DISMAS KALENGA amesema makampuni yote ya ununuzi wa pamba yatanunua pamba hizo katika vyama vya ushirika kama ilivyopangwa na serikali huku jukumu kubwa walilonalo ni kuhakikisha wanasajili vyama vipya.

Hata hivyo KALENGA amesema watatembelea maeneo ya uzalishaji wa pamba ikiwepo kata ya nyankende kutazama uzalishaji wa pamba na kufungua kituo pamoja na kuajiri wahasibu na makarani kwaajili ya zoezi hilo.

Mkutano wa kawaida wa baraza la madiwani wa robo ya tatu Halmashauri ya Ushetu litaendelea tena kesho mei 09 kujadili changamoto mbalimbali na kupitisha maazimio waliyoazimiana madiwani hao.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive