SHIDEFA KAHAMA WAKABIDHIWA BAJAJI ILI KUSAIDIA HUDUMA ZA USAFIRI KWA WAGOJWA



Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Shirika lisilokuwa la Kiserikali la SHIDEPHA + la Mjini KAHAMA limekabidhi pikipiki za magurudumu matatu (bajaji) kwa halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga ili kusaidia huduma za usafiri kwa wagonjwa kwenye zahanati na vituo vya afya vinne vya halmashauri hiyo.

Akikabidhi msaada huo, leo mjini Kahama, Mkurugenzi wa Shirika hilo, VENANCE MZUKA, amesema bajaji hizo, wamezigawa kwenye kituo cha afya Lunguya na Chela , zahanati ya Segese na Isaka na zitasaidia kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu na shughuli zingine za afya.

MZUKA amesema Bajaji hizo zinathamani ya shilingi milioni 28 na kwamba wataendelea kusaidia katika sekta hiyo ya afya katika kata mbalimbali za halmashauri ya Msalala.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Msalala MIBAKO MABUBU amelishukuru shirika la SHIDEPHA + kwa msaada huo na kwamba utasaidia katika shughuli za usafiri kwenye sekta hiyo na huku akiwataka wadau wengine kuendelea kusaidia sekta ya afya kwa manufaa ya jamii.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive