MGODI WA KABELA ILINDI MJINI KAHAMA WAANZA MIKAKATI YA KUPANDA MITI



Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Mgodi wa Kabela ilindi Gold Mine katika Halmashauri ya mji wa KAHAMA mkoani SHINYANGA umeanza mikakati ya kupanda miti wakati wa kiangazi kwa njia ya kisasa ambapo umwagiliaji wake ukakuwa wa matone.

Akizungumza na KAHAMA FM, Mkuu wa Idara ya Afya na Mazingira katika Mgodi huo, MACHIMU NELSON amesema tayari maandalizi yamekwisha kuanza ikiwamo uchimbaji wa mashimo kwaajili ya upandaji wa miche ya miti.

Amesema Kutokana na njia hiyo ya umwagiliaji, Miti yote ikayopandwa wakati wa kiangazi itasitawi vizuri na kwamba wanashirikiana na Ofisi ya mkuu wa wilaya katika kutekeleza zoezi hilo.

MACHIMU amewataka wachimbaji wa madini katika mgodi huo pamoja na wananchi wengine kuendelea kutunza miti katika maeneo hayo pamoja na kudumisha suala la usafi katika maeneo yao.

Mwezi Machi mwaka huu, Mkuu wa wilaya ya Kahama FADHILI NKURLU alizundua kampeni ya upandaji wa miti katika Mgodi wa Kabela Ilindi Gold Mine na kuwataka viongozi wa mgodi huo kufanya zoezi hilo kuwa endelevu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive