AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU NA KUSABABISHA KIFO CHAKE


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Mkazi wa Majengo Mjini KAHAMA, ALPHONCE MASOLA ambaye ni fundi Magari jana amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya kuendesha gari bila leseni na kumgonga mtembea kwa miguu na kumsababishia kifo.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Makahama hiyo, IMAN BATENZI mwendesha Mashitaka wa Polisi SAADA RASHID, amesema Mei 7 mwaka huu Majira ya saa 5 usiku katika barabara ya Ngaya, MASOLA alimgonga CHRISTIAN PAUL na kusababisha kifo chake .

SAADA amefafanua kuwa MASOLO anakabiliwa na mashitaka mawili ambapo katika shitaka la kwanza anadaiwa kuendesha gari katika barabara ya umma bila ya kuwa na leseni ya Udereva kinyume na kifungu namba 40 (1) na 63 (2) (a) ya sheria ya Usalama barabarani.

Katika shitaka la pili anatuhumiwa kuendesha gari kwa mwendokasi na kushindwa kulimudu na kumgonga mtembea kwa miguu na kusababisha kifo chake kinyume na kifungu namba (19) (1) na 113 cha sheria ya usalama barabarani.

MASOLA ambaye katika ajali hiyo alikuwa akiendesha Toyota Land Cruiser pickup T 404 AFR, amekana kutenda kosa hilo ambapo Shauri hilo namba 28/2018 limeahirishwa hadi Mei 24 mwaka huu na amerudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya Dhamana.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive