WAZAZI WILAYANI KAHAMA WAHASWA KUPELEKA WATOTO WAO KUFANYIWA TOHARA


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Wazazi na walezi wenye watoto wenye umri wa miaka 10 hadi 17 ambao hawafanyiwa tohara Wilayani KAHAMA wameshauriwa kuwapeleka watoto wao katika vituo vinavyotoa huduma hiyo bure wakati huu wa Kampeni maalum ya tohara kwa wanaume.

Wito huo umetolewa na DK LAMECK MIHAYO kutoka Zahanati ya BAKWATA Majengo mjini Kahama katika tathimini ya kampeni ya Tohara kwa wanaume inayoendelea katika Halmashauri ya Mji wa Kahama na Msalala kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la Intrahealth.

Amesema watoto hao peke yao hawatoweza kupatiwa huduma hiyo kwa sababu bado umri wao ni mdogo kuweza kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya baada ya kufanyiwa tohara.

Nao baadhi ya watoto waliopatiwa huduma hiyo, FURAHA MICHAEL na ERICK SHIJA wamewaomba wazazi kuwapeleka watoto wenzao kupata huduma hiyo ili kujikinga na magonjwa mbalimbali yakiwemo ya ngono kama vile UKIMWI.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Footprint inayoratibu zoezi hilo, TERENCE MWAKALIKO kiasi cha wanaume 8,400 wanatarajiwa kufanyiwa tohara chini ya kampeni inayoendeshwa katika vituo 10 katika Halmashauri hizo za Kahama mji na Msalala.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive